\id REV - Biblica® Open Kiswahili Contemporary Scriptures (Biblica® Toleo Wazi Neno: Maandiko Matakatifu) \usfm 3.0 \ide UTF-8 \h Ufunuo \toc1 Ufunuo \toc2 Ufunuo \toc3 Ufu \mt1 Ufunuo \c 1 \s1 Utangulizi \p \v 1 Ufunuo wa Isa Al-Masihi aliopewa na Mungu ili awaoneshe watumishi wake mambo ambayo ni lazima yatukie hivi karibuni. Alijulisha mambo haya kwa kumtuma malaika wake kwa Yohana mtumishi wake, \v 2 ambaye anashuhudia kuhusu kila kitu alichokiona, yaani neno la Mungu na ushuhuda wa Isa Al-Masihi. \v 3 Amebarikiwa yeye asomaye maneno ya unabii huu, na wamebarikiwa wale wanaoyasikia na kuyatia moyoni yale yaliyoandikwa humo, kwa sababu wakati umekaribia. \b \s1 Salamu kwa makundi saba ya waumini \po \v 4 Yohana. \po Kwa makundi saba ya waumini yaliyo jimbo la Asia. \po Neema na amani ziwe kwenu kutoka kwake aliyeko, aliyekuwako, na atakayekuja, na kutoka kwa wale roho saba walio mbele ya kiti chake cha enzi, \v 5 na kutoka kwa Isa Al-Masihi, aliye shahidi mwaminifu, mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu, mtawala wa wafalme wa dunia. \p Kwake yeye anayetupenda na aliyetuweka huru kutoka dhambi zetu kwa damu yake, \v 6 na akatufanya sisi kuwa ufalme na makuhani, ili tumtumikie Mungu wake ambaye ni Baba\f + \fr 1:6 \fr*\ft Kwa mwanadamu, Mwenyezi Mungu ni Baba kupitia uhusiano unaopatikana katika kumtumaini Isa Al-Masihi.\ft*\f* yake. Utukufu na uwezo ni vyake milele na milele! Amen. \q1 \v 7 “Tazama! Anakuja na mawingu,” \q2 na “kila jicho litamwona, \q1 hata wale waliomchoma”; \q2 na makabila yote duniani \q2 “yataomboleza kwa sababu yake.” \qc Naam, ndivyo itakavyokuwa! Amen. \b \p \v 8 “Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mwenyezi Mungu, “aliyeko, aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi.” \b \s1 Maono ya Al-Masihi \p \v 9 Mimi, Yohana, ndugu yenu ninayeshiriki pamoja nanyi mateso katika Isa na katika ufalme na uvumilivu katika saburi, nilikuwa katika kisiwa cha Patmo kwa ajili ya neno la Mungu na ushuhuda wa Isa. \v 10 Katika Siku ya Bwana, nilikuwa katika Roho wa Mungu na nikasikia sauti kubwa kama ya baragumu nyuma yangu \v 11 ikisema, “Andika kwenye kitabu haya yote unayoyaona, kisha uyapeleke kwa makundi saba ya waumini: kwa Efeso, Smirna, Pergamo, Thiatira, Sardi, Filadelfia na Laodikia.” \p \v 12 Ndipo nikageuka ili nione ni sauti ya nani iliyokuwa ikisema nami. Nami nilipogeuka, nikaona vinara saba vya taa vya dhahabu, \v 13 na katikati ya vile vinara vya taa, alikuwamo mtu kama Mwana wa Adamu, akiwa amevaa joho refu, na mkanda wa dhahabu ukiwa umefungwa kifuani mwake. \v 14 Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu, nyeupe kama theluji, nayo macho yake yalikuwa kama mwali wa moto. \v 15 Nyayo zake zilikuwa kama shaba inayong’aa katika tanuru la moto, nayo sauti yake ilikuwa kama mngurumo wa maji mengi. \v 16 Katika mkono wake wa kuume alishika nyota saba, na kinywani mwake ulitoka upanga mkali wenye makali kuwili. Uso wake ulikuwa kama jua liking’aa kwa nguvu zake zote. \p \v 17 Nilipomwona, nilianguka miguuni pake kama aliyekufa. Ndipo akauweka mkono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope, Mimi ndiye wa Kwanza na wa Mwisho. \v 18 Mimi ni Yeye Aliye Hai, niliyekuwa nimekufa, na tazama, ni hai milele na milele! Nami ninazo funguo za mauti na Kuzimu\f + \fr 1:18 \fr*\ft Kuzimu kwa Kiyunani ni \ft*\fqa Hades\fqa*\ft , yaani \ft*\fqa mahali pa wafu.\fqa*\f*. \p \v 19 “Basi andika mambo uliyoyaona, yaliyopo na yale yatakayotukia baada ya haya. \v 20 Kuhusu siri ya zile nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kuume na vile vinara saba vya taa vya dhahabu ni hii: Zile nyota saba ni malaika wa yale makundi saba ya waumini, navyo vile vinara saba ni hayo makundi saba. \c 2 \s1 Kwa kundi la waumini lililoko Efeso \p \v 1 “Kwa malaika wa kundi la waumini lililoko Efeso, andika: \b \pi1 Haya ndio maneno ya yule aliyezishika zile nyota saba katika mkono wake wa kuume na ambaye hutembea kati ya vile vinara saba vya taa vya dhahabu. \b \pi1 \v 2 Nayajua matendo yako, bidii yako na saburi yako. Najua kuwa huwezi kuwavumilia watu waovu, na kwamba umewajaribu wale wanaojifanya mitume na kumbe sio, nawe umewatambua kuwa ni waongo. \v 3 Umevumilia na kustahimili taabu kwa ajili ya Jina langu, wala hukuchoka. \v 4 Lakini nina neno dhidi yako: Umeuacha upendo wako wa kwanza. \v 5 Kumbuka basi ni wapi ulikoanguka! Tubu na ukafanye matendo yale ya kwanza. Kama usipotubu, nitakuja kwako na kukiondoa kinara chako cha taa kutoka mahali pake. \v 6 Lakini una jambo hili kwa upande wako: Unayachukia matendo ya Wanikolai, ambayo nami pia nayachukia. \b \pi1 \v 7 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho wa Mungu ayaambia makundi ya waumini. Yeye ashindaye, nitampa haki ya kula matunda ya uzima, ambao uko katika paradiso\f + \fr 2:7 \fr*\ft Paradiso maana yake \ft*\fqa bustani nzuri\fqa*\f* ya Mungu. \s1 Kwa kundi la waumini lililoko Smirna \p \v 8 “Kwa malaika wa kundi la waumini lililoko Smirna, andika: \b \pi1 Haya ndio maneno yake yeye aliye wa Kwanza na wa Mwisho, aliyekufa kisha akafufuka. \b \pi1 \v 9 Naijua dhiki yako na umaskini wako, lakini wewe ni tajiri! Nayajua masingizio ya wale wasemao kuwa ni Wayahudi lakini sio, bali wao ni sinagogi\f + \fr 2:9 \fr*\ft Nyumba ya ibada na mafunzo.\ft*\f* la Shetani. \v 10 Usiogope mateso yatakayokupata. Nakuambia ibilisi atawatia baadhi yenu gerezani ili kuwajaribu, nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji la uzima. \b \pi1 \v 11 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho wa Mungu ayaambia makundi ya waumini. Yeye ashindaye hatadhuriwa kamwe na mauti ya pili. \s1 Kwa kundi la waumini lililoko Pergamo \p \v 12 “Kwa malaika wa kundi la waumini lililoko Pergamo, andika: \b \pi1 Haya ndio maneno yake yeye aliye na upanga mkali wenye makali kuwili. \b \pi1 \v 13 Ninajua unakoishi: kule Shetani ana kiti chake cha utawala. Lakini umelishika Jina langu. Wala hukuikana imani yako kwangu, hata katika siku za shahidi wangu mwaminifu Antipa, ambaye aliuawa katika mji wenu mkuu, anakoishi Shetani. \v 14 Hata hivyo, nina mambo machache dhidi yako: Unao watu wafuatao mafundisho ya Balaamu, yule aliyemfundisha Balaki kuwashawishi Waisraeli watende dhambi kwa kula vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu na kufanya uasherati. \v 15 Vivyo hivyo unao wale wanaoyashikilia mafundisho ya Wanikolai. \v 16 Basi tubu! Ama sivyo, nitakuja kwako upesi na kupigana na watu hao kwa upanga wa kinywa changu. \b \pi1 \v 17 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho wa Mungu ayaambia makundi ya waumini. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa. Nitampa pia jiwe jeupe ambalo juu yake limeandikwa jina jipya asilolijua mtu, isipokuwa yule anayelipokea. \s1 Kwa kundi la waumini lililoko Thiatira \p \v 18 “Kwa malaika wa kundi la waumini lililoko Thiatira, andika: \b \pi1 Haya ndio maneno ya Mwana wa Mungu\f + \fr 2:18 \fr*\ft Yaani Mwana wa asili moja na Mwenyezi Mungu (\+xt Yohana 1:1-2\+xt*), wa kiroho, bali si wa kimwili.\ft*\f*, ambaye macho yake ni kama mwali wa moto, na ambaye miguu yake ni kama shaba iliyosuguliwa. \b \pi1 \v 19 Nayajua matendo yako, upendo wako na imani yako, huduma na saburi yako, na kwamba matendo yako ya sasa yamezidi yale ya kwanza. \v 20 Hata hivyo, nina neno dhidi yako: Unamvumilia yule mwanamke Yezebeli ambaye anajiita nabii, lakini anawafundisha na kuwapotosha watumishi wangu ili wafanye uasherati na kula vyakula vilivyotolewa sadaka kwa sanamu. \v 21 Nimempa muda ili atubu kwa ajili ya uasherati wake, lakini hataki. \v 22 Kwa hiyo nitamtupa kwenye kitanda cha mateso, na nitawafanya hao wanaozini naye kupata mateso makali wasipotubia njia zake. \v 23 Nami nitawaua watoto wake. Nayo makundi yote ya waumini yatajua kwamba Mimi ndiye nichunguzaye mioyo na nia, na kwamba nitamlipa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake. \v 24 Basi nawaambia ninyi wengine mlioko Thiatira, ninyi ambao hamyafuati mafundisho ya Yezebeli, wala hamkujifunza hayo yanayoitwa mambo ya ndani sana ya Shetani (sitaweka mzigo mwingine wowote juu yenu): \v 25 Lakini shikeni sana mlicho nacho, hadi nitakapokuja. \v 26 Atakayeshinda na kutenda mapenzi yangu hadi mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa: \v 27 ‘Atawatawala kwa fimbo ya chuma, atawavunja vipande vipande kama chombo cha udongo’: kama mimi nilivyopokea mamlaka kutoka kwa Baba yangu. \v 28 Nami nitampa pia ile nyota ya asubuhi. \b \pi1 \v 29 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho wa Mungu ayaambia makundi ya waumini. \c 3 \s1 Kwa kundi la waumini lililoko Sardi \p \v 1 “Kwa malaika wa kundi la waumini lililoko Sardi, andika: \b \pi1 Haya ndio maneno ya aliye na zile Roho saba za Mungu\f + \fr 3:1 \fr*\ft Roho saba za Mwenyezi Mungu hapa inamaanisha Roho wa Mungu katika ukamilifu wa utendaji wake.\ft*\f* na zile nyota saba. \b \pi1 Nayajua matendo yako, kwamba una sifa ya kuwa hai, lakini umekufa. \v 2 Amka! Nawe uyaimarishe yale yaliyosalia na yaliyo karibu kufa, kwa maana sikuona kwamba kazi zako zimekamilika machoni pa Mungu wangu. \v 3 Kumbuka basi yale uliyoyapokea na kuyasikia; yatii na ukatubu. Lakini usipoamka, nitakuja kama mwizi wala hutajua saa nitakayokuja kwako. \v 4 Lakini bado una watu wachache katika Sardi ambao hawajayachafua mavazi yao. Wao wataenda pamoja nami, wakiwa wamevaa mavazi meupe, kwa maana wanastahili. \v 5 Yeye ashindaye atavikwa vazi jeupe kama wao. Sitafuta jina lake kutoka kitabu cha uzima, bali nitalikiri jina lake mbele za Baba\f + \fr 3:5 \fr*\ft Jina Baba linaonesha uhusiano maalum wa Isa na Mwenyezi Mungu.\ft*\f* yangu na mbele za malaika wake. \b \pi1 \v 6 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho wa Mungu ayaambia makundi ya waumini. \s1 Kwa kundi la waumini lililoko Filadelfia \p \v 7 “Kwa malaika wa kundi la waumini lililoko Filadelfia, andika: \b \pi1 Haya ndio maneno yake yeye aliye mtakatifu na wa kweli, yeye aliye na ufunguo wa Daudi. Anachokifungua hakuna awezaye kukifunga, wala anachokifunga hakuna awezaye kukifungua. \b \pi1 \v 8 Nayajua matendo yako. Tazama, nimeweka mbele yako mlango uliofunguliwa, wala hakuna awezaye kuufunga. Ninajua kwamba una nguvu kidogo lakini umelishika neno langu wala hukulikana Jina langu. \v 9 Nitawafanya wale wa sinagogi la Shetani, wale ambao husema kuwa ni Wayahudi lakini sio, bali ni waongo, nitawafanya waje wapige magoti miguuni pako, na wakiri kwamba nimekupenda. \v 10 Kwa kuwa umeshika amri yangu ya kuvumilia katika saburi, nitakulinda katika saa ya kujaribiwa inayokuja ulimwenguni pote, ili kuwajaribu wote wanaoishi duniani. \v 11 Ninakuja upesi. Shika sana ulicho nacho, ili mtu asije akalichukua taji lako. \v 12 Yeye ashindaye nitamfanya kuwa nguzo katika Hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo kamwe. Nitaandika juu yake Jina la Mungu wangu na jina la mji mkubwa wa Mungu wangu, Yerusalemu mpya, ambao unashuka kutoka mbinguni kwa Mungu wangu. Nami pia nitaandika juu yake Jina langu jipya. \b \pi1 \v 13 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho wa Mungu ayaambia makundi ya waumini. \s1 Kwa kundi la waumini lililoko Laodikia \p \v 14 “Kwa malaika wa kundi la waumini lililoko Laodikia, andika: \b \pi1 Haya ndio maneno yake yeye aliye Amen, shahidi mwaminifu na wa kweli, mtawala wa uumbaji wote wa Mungu. \b \pi1 \v 15 Nayajua matendo yako, kwamba wewe si baridi wala si moto. Afadhali ungekuwa moto au baridi. \v 16 Hivyo kwa kuwa u vuguvugu, si baridi wala moto, nitakutapika utoke kinywani mwangu. \v 17 Kwa maana unasema: ‘Mimi ni tajiri, nimejilimbikizia mali, wala sihitaji kitu chochote.’ Lakini hutambui kwamba wewe ni mnyonge, wa kuhurumiwa, maskini, kipofu, tena uliye uchi. \v 18 Nakushauri ununue kutoka kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto ili upate kuwa tajiri, na mavazi meupe ili uyavae upate kuficha aibu ya uchi wako, na mafuta ya kupaka macho yako ili upate kuona. \v 19 Wale ninaowapenda, ninawakemea na kuwaadibisha. Hivyo uwe na bidii ukatubu. \v 20 Tazama! Nasimama mlangoni nabisha. Kama mtu yeyote akisikia sauti yangu na kufungua mlango, nitaingia ndani na kula pamoja naye, naye pamoja nami. \v 21 Yeye ashindaye nitampa haki ya kuketi pamoja nami kwenye kiti changu cha enzi, kama vile mimi nilivyoshinda na nikaketi pamoja na Baba yangu kwenye kiti chake cha enzi. \b \pi1 \v 22 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho wa Mungu ayaambia makundi ya waumini.” \c 4 \s1 Kiti cha enzi mbinguni \p \v 1 Baada ya mambo hayo nilitazama, nami nikaona mbele yangu mlango uliokuwa wazi mbinguni. Nayo ile sauti niliyokuwa nimeisikia hapo mwanzo ikisema nami kama tarumbeta ikasema, “Njoo huku, nami nitakuonesha yale ambayo hayana budi kutendeka baada ya haya.” \v 2 Ghafula nilikuwa katika Roho wa Mungu, na hapo mbele yangu palikuwa kiti cha enzi mbinguni, kikiwa kimekaliwa na mtu. \v 3 Aliyekuwa amekikalia alikuwa anaonekana kama yaspi na akiki. Kukizunguka kile kiti cha enzi palikuwa na upinde wa mvua uliong’aa kama zumaridi. \p \v 4 Kukizunguka hicho kiti cha enzi palikuwa na viti vingine ishirini na vinne vya utawala, na juu ya hivyo viti walikuwa wameketi wazee ishirini na wanne. Walivaa mavazi meupe, na walikuwa na taji za dhahabu vichwani mwao. \v 5 Kwenye kile kiti cha enzi palikuwa panatoka miali ya radi, ngurumo na sauti za radi. Mbele ya kiti cha enzi, taa saba zilikuwa zinawaka. Hizi ndizo roho saba\f + \fr 4:5 \fr*\ft Roho saba za Mwenyezi Mungu hapa inamaanisha Roho wa Mungu katika ukamilifu wa utendaji wake.\ft*\f* za Mungu. \v 6 Pia mbele ya kiti cha enzi palikuwa na kile kilichoonekana kama bahari ya kioo, iliyokuwa angavu kama bilauri. \p Katikati, kukizunguka kile kiti cha enzi, kulikuwa na viumbe wanne wenye uhai, wamejaa macho mbele na nyuma. \v 7 Kiumbe wa kwanza mwenye uhai alikuwa kama simba, wa pili alikuwa kama ng’ombe dume, wa tatu alikuwa na uso kama wa mwanadamu, na wa nne alikuwa kama tai anayeruka. \v 8 Kila mmoja wa hawa viumbe wanne wenye uhai alikuwa na mabawa sita, na kujawa na macho pande zote hadi chini ya mabawa. Usiku na mchana hawaachi kusema: \qc “Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, \qc ni Bwana Mungu Mwenyezi, \qc aliyekuwako, aliyeko, na atakayekuja.” \m \v 9 Kila mara viumbe hao wanne wenye uhai wanapomtukuza, kumheshimu na kumshukuru yeye aliyeketi kwenye kile kiti cha enzi, tena aishiye milele na milele, \v 10 wale wazee ishirini na wanne huanguka mbele zake aliyeketi kwenye kiti cha enzi, na kumwabudu yeye aliye hai milele na milele. Huziweka taji zao mbele ya kiti cha enzi, wakisema: \q1 \v 11 “Bwana wetu na Mungu wetu, \q2 wewe unastahili kupokea utukufu \q2 na heshima na uweza, \q1 kwa maana ndiwe uliyeviumba vitu vyote, \q2 na kwa mapenzi yako viliumbwa \q2 na vimekuwako.” \c 5 \s1 Kitabu na Mwana-Kondoo \p \v 1 Kisha nikaona katika mkono wake wa kuume wa yule aliyeketi kwenye kile kiti cha enzi, kitabu kilichoandikwa ndani na nje, kikiwa kimefungwa kwa mihuri saba. \v 2 Nami nikamwona malaika mwenye nguvu akitangaza kwa sauti kuu, “Ni nani anayestahili kuivunja hiyo mihuri na kukifungua kitabu?” \v 3 Lakini hapakuwa na yeyote mbinguni wala duniani au chini ya dunia aliyeweza kukifungua hicho kitabu, wala hata kutazama ndani yake. \v 4 Nikalia sana kwa sababu hakuonekana yeyote anayestahili kukifungua hicho kitabu wala kutazama ndani yake. \v 5 Kisha, mmoja wa wale wazee akaniambia, “Usilie! Tazama, Simba wa kabila la Yuda, wa Uzao wa Daudi, ameshinda. Yeye ndiye anayeweza kukifungua hicho kitabu na kuvunja mihuri yake saba.” \p \v 6 Ndipo nikaona katikati ya kile kiti cha enzi na wale viumbe wenye uhai wanne, na katikati ya wale wazee, Mwana-Kondoo amesimama, akiwa kama amechinjwa. Alikuwa na pembe saba na macho saba, ambazo ndizo zile Roho saba\f + \fr 5:6 \fr*\ft Roho saba za Mwenyezi Mungu hapa inamaanisha Roho wa Mungu katika ukamilifu wa utendaji wake.\ft*\f* za Mungu zilizotumwa duniani pote. \v 7 Huyo Mwana-Kondoo akaja na kukitwaa kile kitabu kutoka mkono wa kuume wa yule aliyeketi kwenye kile kiti cha enzi. \v 8 Alipokwisha kukitwaa kile kitabu, wale viumbe wenye uhai wanne pamoja na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele ya yule Mwana-Kondoo. Kila mmoja wao alikuwa na kinubi, nao walikuwa wameshika mabakuli ya dhahabu yaliyojaa uvumba, ambayo ni maombi ya watakatifu. \v 9 Nao wakaimba wimbo mpya, wakisema: \q1 “Wewe unastahili kukitwaa kitabu \q2 na kuivunja mihuri yake, \q1 kwa sababu ulichinjwa, \q2 na kwa damu yako ukamnunulia Mungu \q2 watu kutoka kila kabila, kila lugha, \q2 kila jamaa na kila taifa. \q1 \v 10 Wewe umewafanya hawa wawe ufalme na makuhani \q2 wa kumtumikia Mungu wetu, \q2 nao watatawala duniani.” \p \v 11 Kisha nikatazama, nikasikia sauti za malaika wengi wakiwa wamekizunguka kile kiti cha enzi, pamoja na wale viumbe wenye uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne. Idadi yao ilikuwa kumi elfu mara kumi elfu na maelfu ya maelfu. \v 12 Nao waliimba kwa sauti kuu, wakisema: \q1 “Anastahili Mwana-Kondoo, yeye aliyechinjwa, \q2 kupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu \q2 na heshima na utukufu na sifa!” \p \v 13 Kisha nikasikia kila kiumbe mbinguni na duniani, chini ya nchi, na baharini, na vyote vilivyomo, vikiimba: \q1 “Sifa na heshima na utukufu na uweza \q2 ni vyake yeye aliyeketi juu ya hicho kiti cha enzi, \q1 na kwa Mwana-Kondoo, \q2 milele na milele!” \m \v 14 Wale viumbe wenye uhai wanne wakasema, “Amen!” Nao wale wazee wakaanguka kifudifudi wakaabudu. \c 6 \s1 Mwana-Kondoo afungua mihuri saba \p \v 1 Nikaangalia Mwana-Kondoo alipofungua ule muhuri wa kwanza miongoni mwa mihuri saba. Ndipo nikasikia mmoja wa wale viumbe wanne wenye uhai akisema kwa sauti kama ya radi: “Njoo!” \v 2 Nikatazama, na hapo mbele yangu palikuwa na farasi mweupe! Yeye aliyempanda alikuwa na upinde, naye akapewa taji, akampanda akatoka akiwa kama mshindi aelekeaye katika kushinda. \p \v 3 Alipouvunja ule muhuri wa pili, nikamsikia yule kiumbe wa pili mwenye uhai akisema, “Njoo!” \v 4 Ndipo akatokea farasi mwingine mwekundu sana. Yeye aliyempanda akapewa uwezo wa kuondoa amani duniani na kuwafanya watu wauane. Yeye akapewa upanga mkubwa. \p \v 5 Mwana-kondoo alipouvunja ule muhuri wa tatu, nikamsikia yule kiumbe wa tatu mwenye uhai akisema, “Njoo!” Nikatazama, na mbele yangu palikuwa na farasi mweusi! Yeye aliyempanda alikuwa na mizani mkononi mwake. \v 6 Ndipo nikasikia kile kilichokuwa kama sauti katikati ya wale viumbe wanne wenye uhai ikisema, “Kipimo kimoja\f + \fr 6:6 \fr*\ft Ni kama lita moja.\ft*\f* cha ngano kwa mshahara wa kibarua wa siku moja\f + \fr 6:6 \fr*\ft Sawa na dinari moja.\ft*\f*, na vipimo vitatu vya shayiri kwa mshahara wa kibarua cha siku moja. Lakini usiharibu mafuta wala divai!” \p \v 7 Alipouvunja ule muhuri wa nne, nikasikia sauti ya yule kiumbe wa nne mwenye uhai ikisema, “Njoo!” \v 8 Nikatazama, na hapo mbele yangu palikuwa na farasi mwenye rangi ya kijivujivu! Yeye aliyempanda aliitwa Mauti, naye Kuzimu\f + \fr 6:8 \fr*\ft Kuzimu kwa Kiyunani ni \ft*\fqa Hades\fqa*\ft , yaani \ft*\fqa mahali pa wafu.\fqa*\f* alikuwa akimfuata nyuma yake kwa karibu. Wakapewa mamlaka juu ya robo ya dunia, kuua kwa upanga, njaa, tauni na kwa wanyama wakali wa dunia. \p \v 9 Mwana-kondoo alipouvunja ule muhuri wa tano, nikaona chini ya madhabahu, roho za wale waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu na kwa ajili ya ushuhuda walioutunza. \v 10 Wakalia kwa sauti kuu, wakasema, “Hata lini, Ee Bwana Mungu Mwenyezi, uliye mtakatifu na mwaminifu, hutawahukumu na kulipiza kisasi kwa watu wanaoishi duniani kwa ajili ya damu yetu?” \v 11 Kisha kila mmoja wao akapewa joho jeupe na wakaambiwa wangoje kwa muda kidogo zaidi, hadi idadi ya ndugu zao na watumishi wenzao watakaouawa kama wao walivyouawa, itakapotimia. \p \v 12 Nikatazama alipouvunja ule muhuri wa sita. Pakatokea tetemeko kuu la ardhi, na jua likawa jeusi kama gunia lililotengenezwa kwa singa za mbuzi, na mwezi wote ukawa mwekundu kama damu. \v 13 Nyota zilizo angani zikaanguka ardhini kama vile matunda ya mtini yasiyokomaa yaangukavyo wakati mti wake unapotikiswa na upepo mkali. \v 14 Anga ikatoweka kama vile karatasi isokotwavyo, na kila mlima na kila kisiwa kikaondolewa mahali pake. \p \v 15 Ndipo wafalme wa dunia, wakuu wote, majemadari, matajiri, wenye nguvu na kila mtu, mtumwa na mtu huru, wakajificha katika mapango na kwenye miamba ya milima. \v 16 Wakaiita milima na miamba wakisema, “Tuangukieni, mkatufiche na uso wake yeye aliyeketi kwenye kile kiti cha enzi, na mkatuepushe na ghadhabu ya Mwana-Kondoo! \v 17 Kwa maana siku ile kuu ya ghadhabu yao imewadia. Je, ni nani awezaye kustahimili?” \c 7 \s1 Waisraeli 144,000 watiwa muhuri \p \v 1 Baada ya hili nikaona malaika wanne wakiwa wamesimama katika pembe nne za dunia, wakizuia hizo pepo nne za dunia, ili pasiwe na upepo utakaovuma juu ya nchi au juu ya bahari au juu ya mti wowote. \v 2 Nikaona malaika mwingine akipanda kutoka mawio ya jua akiwa na muhuri wa Mungu aliye hai. Akawaita kwa sauti kubwa wale malaika wanne waliokuwa wamepewa mamlaka ya kuidhuru nchi na bahari, akisema, \v 3 “Msiidhuru nchi wala bahari, wala miti, hadi tuwe tumetia muhuri kwenye paji za nyuso za watumishi wa Mungu wetu.” \v 4 Ndipo nikasikia idadi ya wale waliotiwa muhuri: elfu mia moja na arobaini na nne kutoka makabila yote ya Israeli. \b \li1 \v 5 Kutoka kabila la Yuda elfu kumi na mbili walitiwa muhuri, \li1 kutoka kabila la Reubeni elfu kumi na mbili, \li1 kutoka kabila la Gadi elfu kumi na mbili, \li1 \v 6 kutoka kabila la Asheri elfu kumi na mbili, \li1 kutoka kabila la Naftali elfu kumi na mbili, \li1 kutoka kabila la Manase elfu kumi na mbili, \li1 \v 7 kutoka kabila la Simeoni elfu kumi na mbili, \li1 kutoka kabila la Lawi elfu kumi na mbili, \li1 kutoka kabila la Isakari elfu kumi na mbili, \li1 \v 8 kutoka kabila la Zabuloni elfu kumi na mbili, \li1 kutoka kabila la Yusufu elfu kumi na mbili, \li1 na kutoka kabila la Benyamini elfu kumi na mbili. \s1 Umati mkubwa wa watu kutoka mataifa yote \p \v 9 Baada ya hili nikatazama na hapo mbele yangu palikuwa na umati mkubwa wa watu ambao hakuna yeyote awezaye kuwahesabu, kutoka kila taifa, kila kabila, kila jamaa na kila lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi na mbele ya Mwana-Kondoo. Walikuwa wamevaa mavazi meupe na wakiwa wameshika matawi ya mitende mikononi mwao. \v 10 Nao walikuwa wakipaza sauti kwa nguvu, wakisema: \q1 “Wokovu una Mungu wetu, \q1 yeye aliyeketi kwenye kile kiti cha enzi, \q1 na Mwana-Kondoo!” \m \v 11 Malaika wote walikuwa wamesimama kukizunguka kile kiti cha enzi na wale wazee, na wale viumbe wanne wenye uhai. Wakaanguka kifudifudi mbele ya hicho kiti cha enzi na kumwabudu Mungu, \v 12 wakisema: \q1 “Amen! \q1 Sifa na utukufu \q1 na hekima na shukrani na heshima \q1 na uweza na nguvu \q1 viwe kwa Mungu wetu milele na milele. \q1 Amen!” \p \v 13 Kisha mmoja wa wale wazee akaniuliza, “Ni nani hawa waliovaa mavazi meupe, nao wametoka wapi?” \p \v 14 Nikamjibu, “Bwana, wewe unajua.” \p Naye akasema, “Hawa ni wale waliotoka katika ile dhiki kuu, nao wamefua mavazi yao katika damu ya Mwana-Kondoo na kuyafanya meupe kabisa. \v 15 Kwa hiyo, \q1 “Wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu \q2 na kumtumikia usiku na mchana \q2 katika Hekalu lake; \q1 naye aliyeketi katika kile kiti cha enzi \q2 atatanda hema lake juu yao. \q1 \v 16 Kamwe hawataona njaa \q2 wala kiu tena. \q1 Jua halitawachoma \q2 wala joto lolote liunguzalo. \q1 \v 17 Kwa maana Mwana-Kondoo \q2 aliyeko katikati ya kile kiti cha enzi \q2 atakuwa Mchungaji wao; \q1 naye atawaongoza kwenda \q2 kwenye chemchemi za maji yaliyo hai. \q1 Naye Mungu atawafuta machozi \q2 kutoka machoni mwao.” \c 8 \s1 Muhuri wa saba na chetezo cha dhahabu \p \v 1 Mwana-Kondoo alipouvunja ule muhuri wa saba, pakawa kimya mbinguni kwa muda wa nusu saa. \p \v 2 Nami nikawaona wale malaika saba wanaosimama mbele za Mungu, nao wakapewa tarumbeta saba. \p \v 3 Malaika mwingine, aliyekuwa na chetezo cha dhahabu, akaja na kusimama mbele ya madhabahu. Akapewa uvumba mwingi ili autoe pamoja na maombi ya watakatifu wote, juu ya yale madhabahu ya dhahabu yaliyo mbele ya kile kiti cha enzi. \v 4 Ule moshi wa uvumba pamoja na yale maombi ya watakatifu, vikapanda juu mbele za Mungu, kutoka mkononi mwa huyo malaika. \v 5 Kisha yule malaika akakichukua kile chetezo, akakijaza moto kutoka kwa yale madhabahu, akautupa juu ya dunia. Pakatokea sauti za radi na ngurumo, miali ya radi na tetemeko la ardhi. \s1 Tarumbeta ya kwanza \p \v 6 Basi wale malaika saba waliokuwa na zile tarumbeta saba wakajiandaa kuzipiga. \p \v 7 Malaika wa kwanza akaipiga tarumbeta yake, pakatokea mvua ya mawe na moto uliochanganyika na damu, navyo vikatupwa kwa nguvu juu ya nchi. Na theluthi ya dunia ikateketea, theluthi ya miti ikateketea, na nyasi yote mbichi ikateketea. \s1 Tarumbeta ya pili \p \v 8 Malaika wa pili akaipiga tarumbeta yake na kitu kama mlima mkubwa unaowaka moto kikatupwa baharini. Theluthi ya bahari ikawa damu, \v 9 theluthi ya viumbe vyenye uhai vilivyoishi baharini vikafa, na theluthi ya meli zikaharibiwa. \s1 Tarumbeta ya tatu \p \v 10 Malaika wa tatu akaipiga tarumbeta yake, na nyota kubwa iliyokuwa ikiwaka kama taa ikaanguka toka angani, ikaangukia theluthi ya mito na chemchemi za maji. \v 11 Nyota hiyo inaitwa Pakanga\f + \fr 8:11 \fr*\ft Pakanga ni mmea chungu sana.\ft*\f*. Theluthi ya maji yakawa machungu na watu wengi wakafa kutokana na maji hayo kwa maana yalikuwa machungu. \s1 Tarumbeta ya nne \p \v 12 Kisha malaika wa nne akaipiga tarumbeta yake, na theluthi ya jua, theluthi ya mwezi na theluthi ya nyota zikapigwa. Kwa hiyo theluthi moja ya mwanga ikawa giza. Theluthi ya mchana ikawa haina mwanga na pia theluthi ya usiku. \p \v 13 Nilipokuwa tena nikitazama, nikamsikia tai mmoja akipaza sauti kwa nguvu, huku akiruka katikati ya anga, akasema, “Ole! Ole! Ole wa watu wanaoishi duniani, kwa sababu ya tarumbeta ambazo malaika hao wengine watatu wanakaribia kuzipiga!” \c 9 \s1 Tarumbeta ya tano \p \v 1 Malaika wa tano akaipiga tarumbeta yake, nami nikaona nyota iliyokuwa imeanguka toka angani hadi ardhini. Nyota hiyo ilipewa ufunguo wa lile Shimo\f + \fr 9:1 \fr*\fqa Abyss \fqa*\ft kwa Kiyunani\ft*\f*. \v 2 Alipolifungua hilo Shimo, moshi ukapanda kutoka humo kama moshi wa tanuru kubwa sana. Jua na anga vikatiwa giza na ule moshi uliotoka katika hilo Shimo. \v 3 Ndipo katika ule moshi wakatoka nzige wakaenda juu ya nchi, nao wakapewa nguvu kama zile za nge wa duniani. \v 4 Wakaambiwa wasidhuru majani ya nchi, wala mmea wala mti wowote, bali wawadhuru tu wale watu ambao hawana muhuri wa Mungu kwenye paji za nyuso zao. \v 5 Wakaruhusiwa kuwatesa kwa muda wa miezi mitano, lakini wasiwaue. Uchungu wa kuuma kwao ulikuwa kama ule wa mtu anapoumwa na nge. \v 6 Katika siku hizo watu watatafuta kifo lakini hawatakiona, watatamani kufa, lakini kifo kitawakimbia. \p \v 7 Wale nzige walikuwa na umbo kama la farasi waliotayarishwa kwa ajili ya vita. Kwenye vichwa vyao kulikuwa na kitu kama taji za dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu. \v 8 Walikuwa na nywele kama za wanawake, na meno yao yalikuwa kama ya simba. \v 9 Walikuwa na dirii kama za chuma, na sauti za mabawa yao zilikuwa kama ngurumo za farasi wengi na magari ya vita mengi yakikimbia vitani. \v 10 Walikuwa na mikia yenye miiba ya kuumia, kama nge. Nguvu yao ya kutesa watu kwa huo muda wa miezi mitano ilikuwa katika mikia yao. \v 11 Walikuwa na mfalme wao, ambaye ni malaika wa lile Shimo, ambaye jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kiyunani ni Apolioni\f + \fr 9:11 \fr*\ft maana ya majina haya ni \ft*\fqa Mharabu\fqa*\ft , yaani \ft*\fqa Yule aharibuye\fqa*\f*. \p \v 12 Ole ya kwanza imepita, bado nyingine mbili zinakuja. \s1 Tarumbeta ya sita \p \v 13 Malaika wa sita akaipiga tarumbeta yake, nami nikasikia sauti ikitoka katika zile pembe za madhabahu ya dhahabu iliyo mbele za Mungu. \v 14 Ile sauti ikamwambia yule malaika wa sita mwenye tarumbeta, “Wafungulie wale malaika wanne waliofungwa kwenye ule mto mkubwa Frati.” \v 15 Basi wale malaika wanne, waliokuwa wamewekwa tayari kwa ajili ya saa hiyo, na siku hiyo, na mwezi huo, na mwaka huo ili wawaue theluthi ya wanadamu wakafunguliwa. \v 16 Idadi ya majeshi wapanda farasi ilikuwa milioni mia mbili. Nilisikia idadi yao. \p \v 17 Hivi ndivyo nilivyowaona hao farasi na wapanda farasi katika maono yangu: Wapanda farasi walivaa dirii vifuani zenye rangi nyekundu sana kama ya moto, na yakuti samawi, na kiberiti. Vichwa vya hao farasi vilikuwa kama vichwa vya simba, na moto, moshi na kiberiti vilitoka vinywani mwao. \v 18 Theluthi ya wanadamu wakauawa kwa mapigo hayo matatu, yaani huo moto, moshi na kiberiti, vilivyotoka kwenye vinywa vya hao farasi. \v 19 Nguvu za hao farasi zilikuwa katika vinywa vyao na kwenye mikia yao, kwa sababu mikia yao ilikuwa kama nyoka, yenye vichwa ambayo waliitumia kudhuru. \p \v 20 Wanadamu waliosalia, ambao hawakuuawa katika mapigo hayo, bado walikataa kutubia kazi za mikono yao na hawakuacha kuabudu mashetani na sanamu za dhahabu, za fedha, za shaba, za mawe na za miti, ambazo haziwezi kuona, kusikia wala kutembea. \v 21 Wala hawakutubu na kuacha matendo yao ya uuaji, uchawi, uasherati wala wizi wao. \c 10 \s1 Malaika na kijitabu \p \v 1 Kisha nikamwona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa amevikwa wingu na upinde wa mvua juu ya kichwa chake. Uso wake uling’aa kama jua na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto. \v 2 Mkononi mwake alikuwa ameshika kijitabu kilichokuwa kimefunguliwa. Akauweka mguu wake wa kuume juu ya bahari na mguu wake wa kushoto akauweka juu ya nchi kavu. \v 3 Naye akapaza sauti kwa nguvu kama simba anayenguruma. Aliponguruma, zile radi saba zikatoa ngurumo zake. \v 4 Nazo zile radi saba zilipotoa ngurumo, nilitaka kuanza kuandika, lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Yatie muhuri hayo yaliyosemwa na hizo radi saba na usiyaandike.” \p \v 5 Kisha yule malaika niliyekuwa nimemwona akiwa amesimama juu ya bahari na juu ya nchi akainua mkono wake wa kuume kuelekea mbinguni. \v 6 Naye akaapa kwa Yule aishiye milele na milele, aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, dunia na vyote viijazavyo, pamoja na bahari na vyote vilivyomo, akasema, “Hakuna kungoja tena! \v 7 Lakini katika siku zile huyo malaika wa saba atakaribia kuipiga hiyo tarumbeta yake, siri ya Mungu itatimizwa, kama vile alivyowatangazia watumishi wake manabii.” \p \v 8 Ndipo ile sauti niliyokuwa nimeisikia kutoka mbinguni ikasema nami tena, ikaniambia, “Nenda, chukua kile kitabu kilichofunguliwa kilichoko mkononi mwa yule malaika aliyesimama juu ya bahari na juu ya nchi kavu.” \p \v 9 Basi nikamwendea nikamwomba yule malaika anipe kile kijitabu. Akaniambia, “Chukua na ukile. Kitakuwa kichungu tumboni mwako, lakini kinywani mwako kitakuwa kitamu kama asali.” \v 10 Hivyo nikakichukua kile kijitabu kutoka mkononi mwa yule malaika, nikakila. Kilikuwa kitamu kama asali kinywani mwangu, lakini baada ya kukila, tumbo langu likatiwa uchungu. \v 11 Kisha nikaambiwa, “Imekupasa kutoa unabii tena kuhusu makabila mengi, mataifa, lugha na wafalme.” \c 11 \s1 Mashahidi wawili \p \v 1 Ndipo nikapewa mwanzi uliokuwa kama ufito wa kupimia, nikaambiwa, “Nenda ukapime Hekalu la Mungu pamoja na madhabahu, nawe uwahesabu wale waabuduo humo. \v 2 Lakini usiupime ua wa nje wa Hekalu; uache, kwa sababu ua huo wamepewa watu wa Mataifa. Hao wataukanyagakanyaga mji mtakatifu kwa muda wa miezi arobaini na mbili. \v 3 Nami nitawapa mashahidi wangu wawili uwezo, nao watoe unabii kwa muda wa siku elfu moja mia mbili na sitini, wakiwa wamevaa gunia.” \v 4 Hawa ndio ile mizeituni miwili na vile vinara viwili vya taa visimamavyo mbele za Mwenyezi Mungu, Mungu wa dunia yote. \v 5 Kama mtu yeyote akitaka kuwadhuru, moto hutoka vinywani mwao na kuwateketeza adui zao. Hivi ndivyo impasavyo kufa mtu yeyote atakayetaka kuwadhuru. \v 6 Watu hawa wanao uwezo wa kufunga anga ili mvua isinyeshe wakati wote watakapokuwa wanatoa unabii wao. Nao watakuwa na uwezo wa kuyabadili maji kuwa damu na kuipiga dunia kwa kila aina ya mapigo mara kwa mara kama watakavyo. \p \v 7 Basi watakapokuwa wamemaliza ushuhuda wao, yule mnyama atokaye katika lile Shimo atapigana nao vita, atawashinda na kuwaua. \v 8 Maiti zao zitabaki katika barabara ya mji mkubwa\f + \fr 11:8 \fr*\ft yaani \ft*\fqa Yerusalemu\fqa*\f*, ambao kwa fumbo unaitwa Sodoma na Misri, ambapo pia Isa Bwana wao alisulubiwa. \v 9 Kwa muda wa siku tatu na nusu, watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa wataziangalia hizo maiti zao na hawataruhusu zizikwe. \v 10 Watu wanaoishi duniani watazitazama maiti za hao manabii wawili kwa furaha, na kushangilia kwa kupeana zawadi, kwa sababu hao manabii waliwatesa watu wanaoishi duniani. \p \v 11 Lakini baada ya zile siku tatu na nusu, pumzi ya uhai kutoka kwa Mungu ikawaingia, nao wakasimama kwa miguu yao na wote waliowaona wakaingiwa na hofu kuu. \v 12 Kisha wale manabii wawili wakasikia sauti kuu kutoka mbinguni ikiwaambia, “Njooni huku juu!” Nao wakapaa mbinguni katika wingu, wakati adui zao wakiwa wanawatazama. \p \v 13 Saa hiyo hiyo, kukawa na tetemeko kubwa la ardhi na sehemu ya kumi ya mji ikaanguka. Watu elfu saba wakauawa katika tetemeko hilo, nao walionusurika wakaogopa sana, wakamtukuza Mungu wa mbinguni. \p \v 14 Ole ya pili imekwisha kupita, tazama ole ya tatu inakuja upesi. \s1 Tarumbeta ya saba \p \v 15 Yule malaika wa saba akaipiga tarumbeta yake, pakawa na sauti kubwa mbinguni iliyosema: \q1 “Ufalme wa ulimwengu umekuwa \q2 ufalme wa Bwana wetu na wa Al-Masihi wake, \q2 naye atatawala milele na milele.” \m \v 16 Nao wale wazee ishirini na wanne, waliokuwa wameketi mbele za Mungu, kwenye viti vyao vya utawala, wakaanguka kifudifudi, wakamwabudu Mungu, \v 17 wakisema: \q1 “Tunakushukuru, Bwana Mungu Mwenyezi, \q2 uliyeko na uliyekuwako, \q1 kwa kuwa umetwaa uweza wako mkuu \q2 na ukaanza kutawala. \q1 \v 18 Mataifa walikasirika; \q2 nao wakati wa ghadhabu yako umewadia. \q1 Wakati umewadia wa kuwahukumu waliokufa, \q2 na kuwapa thawabu watumishi wako manabii, \q1 na watakatifu wako pamoja na wale wote \q2 wanaoliheshimu Jina lako, \q2 wakubwa kwa wadogo: \q1 na kuwaangamiza wale wanaoiangamiza dunia.” \p \v 19 Ndipo Hekalu la Mungu lililoko mbinguni likafunguliwa, na Sanduku la Agano lake likaonekana humo. Kukatokea miali ya radi, ngurumo, sauti za radi, tetemeko la ardhi na mvua kubwa ya mawe. \c 12 \s1 Mwanamke na joka \p \v 1 Kukaonekana ishara kuu mbinguni: Palikuwa na mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na taji lenye nyota kumi na mbili lilikuwa kichwani mwake. \v 2 Alikuwa na mimba naye akilia kwa uchungu kwa kuwa alikuwa anakaribia kuzaa. \v 3 Kisha ishara nyingine ikaonekana mbinguni: Likaonekana joka kubwa jekundu lenye vichwa saba na pembe kumi, na taji saba katika vichwa vyake. \v 4 Mkia wake ukakokota theluthi ya nyota zote angani na kuziangusha katika nchi. Ndipo lile joka likasimama mbele ya yule mwanamke aliyekuwa karibu kuzaa ili lipate kumla huyo mtoto mara tu atakapozaliwa. \v 5 Yule mwanamke akazaa mtoto wa kiume, atakayeyatawala mataifa yote kwa fimbo ya utawala ya chuma. Lakini huyo mtoto akanyakuliwa na kupelekwa kwa Mungu kwenye kiti chake cha enzi. \v 6 Yule mwanamke akakimbilia jangwani, ambako Mungu alikuwa amemtayarishia mahali ili apate kutunzwa huko kwa muda wa siku elfu moja mia mbili na sitini. \s1 Malaika Mikaeli amshinda joka \p \v 7 Basi palikuwa na vita mbinguni: Mikaeli na malaika wake wakapigana na hilo joka, nalo joka pamoja na malaika wake likapigana nao. \v 8 Lakini joka na malaika wake wakashindwa, na hapakuwa tena na nafasi yao huko mbinguni. \v 9 Lile joka kuu likatupwa chini, yule nyoka wa zamani aitwaye ibilisi au Shetani, aupotoshaye ulimwengu wote. Akatupwa chini duniani, yeye pamoja na malaika wake. \s1 Ushindi mbinguni watangazwa \p \v 10 Kisha nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema: \q1 “Sasa wokovu na uweza na ufalme wa Mungu wetu Mwenyezi umekuja, \q2 na mamlaka ya Al-Masihi wake. \q1 Kwa kuwa ametupwa chini \q2 mshtaki wa ndugu zetu, \q1 anayewashtaki mbele za Mungu \q2 usiku na mchana. \q1 \v 11 Nao wakamshinda \q2 kwa damu ya Mwana-Kondoo \q2 na kwa neno la ushuhuda wao. \q1 Wala wao hawakuyapenda maisha yao sana, \q2 hata wakawa tayari kufa. \q1 \v 12 Kwa hiyo furahini, ninyi mbingu \q2 na wote wanaoishi humo! \q1 Lakini ole wenu nchi na bahari, \q2 kwa maana huyo ibilisi ameshuka kwenu, \q1 akiwa amejaa ghadhabu, \q2 kwa sababu anajua ya kuwa \q2 muda wake ni mfupi!” \p \v 13 Lile joka lilipoona kuwa limetupwa chini duniani, lilimfuatilia yule mwanamke aliyekuwa amezaa mtoto wa kiume. \v 14 Lakini huyo mwanamke akapewa mabawa mawili ya tai mkubwa, kusudi aweze kuruka hadi mahali palipotayarishwa kwa ajili yake huko jangwani, ambako atatunzwa kwa wakati na nyakati na nusu, ya wakati ambako lile joka haliwezi kufika. \v 15 Ndipo lile joka likamwaga maji kama mto kutoka kinywani mwake, ili kumfikia huyo mwanamke, achukuliwe na mafuriko. \v 16 Lakini nchi ikamsaidia huyo mwanamke kwa kufungua kinywa na kuumeza huo mto ambao lile joka lilikuwa limeutoa kinywani mwake. \v 17 Kisha lile joka likapatwa na hasira kali kwa ajili ya huyo mwanamke na likaondoka ili kupigana vita na wazawa waliosalia wa huyo mwanamke, yaani wale wanaozitii amri za Mungu na kuushika ushuhuda wa Isa Al-Masihi. \c 13 \p \v 1 Lile joka likasimama kwenye mchanga wa bahari. \s1 Mnyama kutoka baharini \p Nami nikamwona mnyama akitoka ndani ya bahari. Mnyama huyo alikuwa na pembe kumi na vichwa saba, akiwa na taji kumi kwenye hizo pembe zake, na juu ya kila kichwa kulikuwa na jina la kukufuru. \v 2 Mnyama yule niliyemwona alifanana na chui, lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kichwa chake kama cha simba. Lile joka likampa huyo mnyama nguvu zake, kiti chake cha utawala na mamlaka makubwa. \v 3 Mojawapo ya vichwa vya huyo mnyama kilikuwa kama kilichokwisha kupata jeraha la mauti, lakini jeraha hilo la mauti likapona. Ulimwengu wote ukashangaa ukamfuata huyo mnyama. \v 4 Watu wakaliabudu lile joka kwa sababu lilikuwa limempa huyo mnyama mamlaka yake, pia wakamwabudu huyo mnyama na kuuliza, “Ni nani aliye kama huyu mnyama? Ni nani awezaye kupigana vita naye?” \p \v 5 Huyo mnyama akapewa mdomo wa kusema maneno ya kiburi na kukufuru, na uwezo wa kutumia mamlaka yake kwa muda wa miezi arobaini na mbili. \v 6 Akafungua kinywa chake ili kumkufuru Mungu, akilitukana Jina lake na mahali aishipo na wale wanaokaa mbinguni. \v 7 Pia akaruhusiwa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda. Akapewa uwezo juu ya watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa. \v 8 Nao watu wote wanaoishi duniani watamwabudu huyo mnyama: wale wote ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo, aliyechinjwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu. \p \v 9 Yeye aliye na sikio na asikie. \q1 \v 10 “Ikiwa mtu ni wa kuchukuliwa mateka, \q2 atachukuliwa mateka. \q1 Ikiwa mtu ni wa kuuawa kwa upanga, \q2 atauawa kwa upanga.” \m Hapa ndipo penye wito wa subira na imani ya watakatifu. \s1 Mnyama kutoka ardhini \p \v 11 Kisha nikamwona mnyama mwingine, akipanda juu kutoka ardhini. Alikuwa na pembe mbili kama mwana-kondoo, lakini akanena kama joka. \v 12 Akatumia mamlaka yote ya yule mnyama wa kwanza kwa niaba yake, naye akaifanya dunia na wote walioishi duniani kumwabudu yule mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona. \v 13 Naye akafanya ishara kuu na za ajabu, hata kusababisha moto kushuka toka mbinguni kuja duniani watu wakiona waziwazi. \v 14 Kwa sababu ya zile ishara alizokuwa amepewa uwezo wa kuzifanya kwa niaba ya yule mnyama wa kwanza, akawadanganya watu walioishi duniani. Akawaamuru wasimamishe sanamu kwa heshima ya yule mnyama aliyekuwa amejeruhiwa kwa upanga lakini akaishi. \v 15 Akapewa uwezo wa kuipa pumzi ile sanamu ya yule mnyama wa kwanza, ili iweze kusema na kuwasababisha wale wote waliokataa kuiabudu hiyo sanamu kuuawa. \v 16 Pia alimlazimisha kila mmoja, mdogo na mkubwa, tajiri na maskini, mtu huru na mtumwa, atiwe chapa kwenye mkono wake wa kuume au kwenye paji la uso wake, \v 17 ili mtu yeyote asiweze kununua wala kuuza isipokuwa amekuwa na hiyo chapa, ambayo ni jina la huyo mnyama au tarakimu za jina lake. \p \v 18 Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na ufahamu na ahesabu tarakimu za huyo mnyama, kwa maana ni tarakimu za kibinadamu. Tarakimu zake ni mia sita sitini na sita (666). \c 14 \s1 Mwana-Kondoo na wale 144,000 \p \v 1 Kisha nikatazama, na hapo mbele yangu Mwana-Kondoo alikuwa amesimama juu ya Mlima Sayuni. Pamoja naye walikuwa wale elfu mia moja na arobaini na nne wenye jina la Mwana-Kondoo na jina la Baba\f + \fr 14:1 \fr*\ft Jina Baba linaonesha uhusiano maalum wa Isa na Mwenyezi Mungu.\ft*\f* yake limeandikwa kwenye paji za nyuso zao. \v 2 Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni kama sauti ya maji mengi yaendayo kwa kasi na sauti kama ngurumo ya radi. Sauti hiyo niliyoisikia ilikuwa kama sauti ya wapiga vinubi wakipiga vinubi vyao. \v 3 Nao wakaimba wimbo mpya mbele ya hicho kiti cha enzi, na mbele ya wale viumbe wanne wenye uhai, na wale wazee. Hakuna mtu yeyote aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao elfu mia moja na arobaini na nne waliokuwa wamekombolewa kutoka duniani. \v 4 Hawa ndio wale ambao hawakujitia unajisi kwa wanawake, kwa kuwa wao ni bikira. Wao humfuata Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamekombolewa kutoka miongoni mwa wanadamu wakawa malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo. \v 5 Vinywani mwao hapakuonekana uongo, wala hawakuwa na hatia yoyote. \s1 Malaika watatu \p \v 6 Kisha nikamwona malaika mwingine akiruka juu angani, naye alikuwa na Injili ya milele ya kuwatangazia wale wanaoishi duniani: kwa kila taifa, kabila, lugha na jamaa. \v 7 Akasema kwa sauti kubwa, “Mcheni Mungu na kumpa utukufu, kwa maana saa ya hukumu yake imewadia. Mwabuduni yeye aliyeziumba mbingu, dunia, bahari na chemchemi za maji.” \p \v 8 Malaika wa pili akafuata akisema, “Umeanguka! Umeanguka Babeli Mkuu, mji ule ulioyafanya mataifa yote kulewa kwa mvinyo wa ghadhabu ya uasherati wake.” \p \v 9 Malaika wa tatu akawafuata hao wawili akisema kwa sauti kubwa, “Kama mtu yeyote anamwabudu huyo mnyama na sanamu yake na kutiwa chapa yake kwenye paji la uso wake au kwenye mkono wake, \v 10 yeye pia atakunywa mvinyo wa hasira kali ya Mungu ambayo imemiminwa katika kikombe cha ghadhabu yake pasipo kuchanganywa na maji. Naye atateswa kwa moto uwakao na kiberiti mbele ya malaika watakatifu na mbele za Mwana-Kondoo. \v 11 Nao moshi wa mateso yao hupanda juu milele na milele. Hakuna mapumziko, mchana wala usiku, kwa wale wamwabuduo huyo mnyama na sanamu yake, au kwa yeyote anayepokea chapa ya jina lake.” \v 12 Hapa ndipo penye wito wa subira na uvumilivu wa watakatifu; wale wanaozishika amri za Mungu na kudumu katika uaminifu kwa Isa. \p \v 13 Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika: Wamebarikiwa wafu wafao katika Isa Bwana tangu sasa.” \p “Naam,” asema Roho wa Mungu, “watapumzika kutoka taabu zao, kwa kuwa matendo yao yatawafuata.” \s1 Kuvuna mavuno ya dunia \p \v 14 Nikatazama, hapo mbele yangu palikuwa na wingu jeupe, na aliyekuwa ameketi juu ya hilo wingu alikuwa kama Mwana wa Adamu, akiwa na taji la dhahabu kichwani mwake na mundu mkali mkononi mwake. \v 15 Kisha malaika mwingine akaja kutoka Hekaluni naye akamwita kwa sauti kubwa yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akasema, “Chukua mundu wako ukavune kwa kuwa wakati wa mavuno umewadia, kwa maana mavuno ya dunia yamekomaa.” \v 16 Hivyo yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akauzungusha mundu wake duniani, nayo dunia ikavunwa. \p \v 17 Malaika mwingine akatoka katika Hekalu lililoko mbinguni, naye pia alikuwa na mundu mkali. \v 18 Kisha malaika mwingine, aliyekuwa na mamlaka juu ya moto, akatoka kwenye madhabahu, naye akamwita yule malaika mwenye mundu mkali kwa sauti kubwa, akisema, “Chukua mundu wako mkali ukakusanye vichala vya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva.” \v 19 Hivyo yule malaika akauzungusha mundu wake duniani na kukusanya zabibu za dunia na kuzitupa kwenye shinikizo kubwa la ghadhabu ya Mungu. \v 20 Lile shinikizo likakanyagwa nje ya mji, nayo damu ikatiririka kama mafuriko kutoka hilo shinikizo kufikia kimo cha hatamu za farasi\f + \fr 14:20 \fr*\ft ni kama mita moja na nusu\ft*\f*, kwa umbali wa maili mia moja na themanini\f + \fr 14:20 \fr*\ft yamkini kilomita mia tatu na ishirini\ft*\f*. \c 15 \s1 Malaika saba na mapigo saba \p \v 1 Ndipo nikaona ishara nyingine kubwa ya ajabu mbinguni: malaika saba wenye yale mapigo saba ya mwisho, kwa sababu kwa mapigo hayo ghadhabu ya Mungu ilikuwa imekamilika. \v 2 Nikaona kile kilichoonekana kama bahari ya kioo iliyochanganyikana na moto. Kando ya hiyo bahari, walikuwa wamesimama wale watu waliomshinda yule mnyama na sanamu yake pamoja na tarakimu ya jina lake. Mikononi mwao walikuwa wameshika vinubi walivyopewa na Mungu. \v 3 Nao wakaimba wimbo wa Musa, mtumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakisema: \q1 “Bwana Mungu Mwenyezi, \q2 matendo yako ni makuu na ya ajabu. \q1 Njia zako wewe ni za haki na za kweli, \q2 Mfalme wa nyakati zote! \q1 \v 4 Ni nani ambaye hatakuogopa wewe Mwenyezi Mungu \q2 na kulitukuza jina lako? \q1 Kwa kuwa wewe peke yako ndiwe mtakatifu. \q1 Mataifa yote yatakuja \q2 na kuabudu mbele zako, \q1 kwa kuwa matendo yako ya haki \q2 yamedhihirishwa.” \p \v 5 Baada ya haya nikatazama, nalo Hekalu la Hema la Ushuhuda lilikuwa limefunguliwa mbinguni. \v 6 Ndani ya lile Hekalu wakatoka malaika saba wakiwa na mapigo saba. Walikuwa wamevaa nguo safi za kitani iliyong’aa, na kufungwa mikanda ya dhahabu vifuani mwao. \v 7 Ndipo mmoja wa wale viumbe wanne wenye uhai akawapa wale malaika saba mabakuli saba ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, yeye aishiye milele na milele. \v 8 Nalo lile Hekalu lilijawa na moshi uliotokana na utukufu wa Mungu na uweza wake, wala hakuna yeyote aliyeweza kuingia mle Hekaluni hadi yale mapigo saba ya wale malaika saba yalipomalizika. \c 16 \s1 Mabakuli saba ya ghadhabu ya Mwenyezi Mungu \p \v 1 Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mle Hekaluni ikiwaambia wale malaika saba, “Nendeni, mkayamwage duniani hayo mabakuli saba ya ghadhabu ya Mungu.” \p \v 2 Malaika wa kwanza akaenda akalimwaga hilo bakuli lake juu ya nchi. Majipu mabaya yenye maumivu makali yakawapata wale watu wote waliokuwa na chapa ya yule mnyama na walioabudu sanamu yake. \p \v 3 Malaika wa pili akalimwaga bakuli lake baharini, nayo ikabadilika kuwa damu kama ya mtu aliyekufa na kila kiumbe hai kilichokuwa ndani ya bahari kikafa. \p \v 4 Malaika wa tatu akalimwaga bakuli lake katika mito na chemchemi za maji, nazo zikawa damu. \v 5 Ndipo nikamsikia malaika msimamizi wa maji akisema: \q1 “Wewe una haki katika hukumu hizi ulizotoa, \q2 wewe uliyeko, uliyekuwako, Uliye Mtakatifu, \q2 kwa sababu umehukumu hivyo; \q1 \v 6 kwa kuwa walimwaga damu ya watakatifu wako \q2 na manabii wako, \q1 nawe umewapa damu wanywe \q2 kama walivyostahili.” \m \v 7 Nikasikia madhabahu ikiitikia, \q1 “Naam, Bwana Mungu Mwenyezi, \q2 hukumu zako ni kweli na haki.” \p \v 8 Malaika wa nne akamimina bakuli lake kwenye jua, nalo likapewa nguvu za kuwaunguza watu kwa moto. \v 9 Watu wakaunguzwa na hilo joto kali, wakalaani Jina la Mungu, aliyekuwa na uwezo juu ya mapigo haya, tena wakakataa kutubu na kumtukuza Mungu. \p \v 10 Malaika wa tano akamimina bakuli lake kwenye kiti cha utawala cha yule mnyama, nao ufalme wake ukagubikwa na giza. Watu wakatafuna ndimi zao kwa ajili ya maumivu, \v 11 wakamlaani Mungu wa mbinguni kwa sababu ya maumivu na majeraha yao, wala hawakutubu kwa ajili ya matendo yao maovu. \p \v 12 Malaika wa sita akamimina bakuli lake kwenye mto mkubwa Frati, maji yake yakakauka ili kutayarisha njia kwa ajili ya wafalme kutoka Mashariki. \v 13 Kisha nikaona roho wachafu watatu waliofanana na vyura wakitoka katika kinywa cha lile joka na katika kinywa cha yule mnyama na katika kinywa cha yule nabii wa uongo. \v 14 Hizo ndizo roho za pepo wachafu zitendazo miujiza. Nazo huwaendea wafalme wa ulimwengu wote na kuwakusanya tayari kwa ajili ya vita katika siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi. \b \mi \v 15 “Tazama, naja kama mwizi! Amebarikiwa yeye akeshaye na kuziweka tayari nguo zake ili asiende uchi na kuonekana aibu yake.” \b \m \v 16 Ndipo wakawakusanya wafalme pamoja mahali paitwapo Har-Magedoni kwa Kiebrania. \p \v 17 Malaika wa saba akamimina bakuli lake angani na sauti kubwa ikatoka mle Hekaluni katika kile kiti cha enzi, ikisema, “Imekwisha kuwa!” \v 18 Kukawa na miali ya radi, ngurumo, radi na tetemeko kubwa la ardhi. Hapajawahi kuwa na tetemeko la ardhi kama hilo tangu mwanadamu awepo duniani, kwani lilikuwa tetemeko kubwa ajabu. \v 19 Ule mji mkubwa ukagawanyika katika sehemu tatu, nayo miji ya mataifa ikaanguka. Mungu akakumbuka Babeli Mkuu na kumpa kikombe kilichojaa mvinyo wa ghadhabu ya hasira yake. \v 20 Kila kisiwa kikatoweka wala milima haikuonekana. \v 21 Mvua kubwa ya mawe yenye uzito wa talanta moja\f + \fr 16:21 \fr*\ft Talanta moja ni kama kilo 34.\ft*\f* ikashuka kutoka mbinguni, ikawaangukia wanadamu. Nao wanadamu wakamlaani Mungu kwa ajili ya hayo mapigo ya mvua ya mawe, kwa sababu pigo hilo lilikuwa la kutisha. \c 17 \s1 Kahaba mkuu na mnyama \p \v 1 Mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na yale mabakuli saba akaja akaniambia, “Njoo, nitakuonesha adhabu ya yule kahaba mkuu, aliyeketi juu ya maji mengi. \v 2 Yule ambaye wafalme wa dunia walizini naye na watu walioishi duniani walilewa kwa mvinyo wa uzinzi wake.” \p \v 3 Kisha yule malaika akanichukua katika Roho wa Mungu, akanipeleka jangwani. Huko nikamwona mwanamke mmoja ameketi juu ya mnyama mwekundu aliyejaa majina ya kumkufuru Mungu mwili mzima. Mnyama huyo alikuwa na vichwa saba na pembe kumi. \v 4 Huyo mwanamke alikuwa amevaa mavazi ya rangi ya zambarau na nyekundu, akimetameta kwa dhahabu, vito vya thamani na lulu. Mkononi mwake alikuwa ameshika kikombe cha dhahabu kilichojaa mambo ya machukizo na uchafu wa uzinzi wake. \v 5 Kwenye paji lake la uso palikuwa pameandikwa jina la siri: \pc \sc Babeli Mkuu,\sc* \pc \sc Mama wa makahaba\sc* \pc \sc na wa machukizo ya dunia.\sc* \m \v 6 Nikaona kuwa huyo mwanamke alikuwa amelewa kwa damu ya watakatifu, yaani damu ya wale watu waliouawa kwa ushuhuda wa Isa. \p Nilipomwona huyo mwanamke, nilistaajabu sana. \v 7 Ndipo yule malaika akaniambia, “Kwa nini unastaajabu? Nitakufafanulia siri ya huyo mwanamke na huyo mnyama aliyempanda, mwenye vichwa saba na pembe kumi. \v 8 Huyo mnyama ambaye ulimwona awali alikuwako, lakini sasa hayuko, naye atapanda kutoka lile Shimo na kwenda kwenye maangamizi yake. Watu wanaoishi duniani ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima tangu kuumbwa kwa ulimwengu watastaajabu kumwona huyo mnyama, kwa maana alikuwako hapo awali, na sasa hayuko, lakini atakuwako baadaye. \p \v 9 “Hapa ndipo penye wito wa akili pamoja na hekima. Vile vichwa saba ni vilima saba ambavyo huyo mwanamke amevikalia. \v 10 Pia hivyo vichwa saba ni wafalme saba. Watano wamekwisha kuanguka, mmoja yupo, mwingine hajaja bado, lakini atakapokuja atalazimika kukaa kwa muda mfupi. \v 11 Yule mnyama aliyekuwako hapo awali na sasa hayuko, yeye ni mfalme wa nane. Ni miongoni mwa wale saba, naye anaenda kwenye maangamizi yake. \p \v 12 “Zile pembe kumi ulizoziona ni wafalme kumi ambao bado hawajapokea ufalme, lakini watapokea mamlaka kuwa wafalme kwa saa moja pamoja na yule mnyama. \v 13 Hawa wana nia moja, nao watamwachia yule mnyama nguvu zao na mamlaka yao. \v 14 Watafanya vita na Mwana-Kondoo, lakini Mwana-Kondoo atawashinda kwa sababu yeye ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme. Yeye atakuwa pamoja na watu wake walioitwa ambao ni wateule wake na wafuasi wake waaminifu.” \p \v 15 Kisha yule malaika akaniambia, “Yale maji uliyoyaona yule kahaba akiwa ameketi juu yake ni jamaa, makundi ya watu, mataifa na lugha. \v 16 Zile pembe kumi ulizoziona, pamoja na huyo mnyama, watamchukia huyo kahaba, watamfilisi na kumwacha uchi, watamla nyama yake na kumteketeza kwa moto. \v 17 Kwa maana Mungu ameweka mioyoni mwao kutimiza kusudi lake kwa kukubali kumpa yule mnyama mamlaka yao ya utawala hadi maneno ya Mungu yatakapotimia. \v 18 Yule mwanamke uliyemwona ni ule mji mkubwa unaowatawala wafalme wa dunia.” \c 18 \s1 Kuanguka kwa Babeli \p \v 1 Baada ya haya nikaona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni, akiwa na mamlaka kuu na dunia ikaangazwa kwa mng’ao wake. \v 2 Naye akapaza sauti kwa nguvu, akisema: \q1 “ ‘Umeanguka! Umeanguka Babeli Mkuu!’ \q2 Umekuwa makao ya mashetani \q1 na makazi ya kila pepo mchafu, \q2 makazi ya kila ndege na kila mnyama achukizaye. \q1 \v 3 Kwa maana mataifa yote yamekunywa \q2 mvinyo wa ghadhabu ya uasherati wake. \q1 Nao wafalme wa dunia wamefanya uzinzi naye, \q2 na wafanyabiashara wa dunia \q2 wametajirika kutokana na wingi wa utajiri wake.” \p \v 4 Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni ikisema: \q1 “ ‘Tokeni katikati yake, enyi watu wangu,’ \q2 ili msije mkashiriki dhambi zake, \q2 ili msije mkapatwa na pigo lake lolote; \q1 \v 5 kwa kuwa dhambi zake zimefika hadi mbinguni, \q2 naye Mungu ameukumbuka uhalifu wake. \q1 \v 6 Mtendee kama yeye alivyotenda; \q2 umlipe mara mbili kwa ajili ya yale aliyotenda. \q1 Katika kikombe chake mchanganyie \q2 mara mbili ya kile alichochanganya. \q1 \v 7 Mpatie mateso na huzuni nyingi sawa na \q2 utukufu na anasa alizojipatia. \q1 Kwa kuwa moyoni mwake hujivuna, akisema, \q2 ‘Mimi ninatawala kama malkia; \q2 mimi si mjane, wala sitaona huzuni kamwe.’ \q1 \v 8 Kwa hiyo mapigo yatampata kwa siku moja: \q2 mauti, maombolezo na njaa. \q1 Naye atateketezwa kwa moto, \q2 kwa maana Mwenyezi Mungu amhukumuye ana nguvu. \p \v 9 “Wafalme wa dunia waliozini naye na kushiriki anasa zake watakapoona moshi wa kuungua kwake, watamlilia na kumwombolezea. \v 10 Kwa hofu kubwa ya mateso yake, watasimama mbali na kulia na wakisema: \q1 “ ‘Ole! Ole, ee mji mkubwa, \q2 ee Babeli mji wenye nguvu! \q1 Hukumu yako imekuja katika saa moja!’ \p \v 11 “Wafanyabiashara wa dunia watalia na kumwomboleza kwa sababu hakuna anunuaye bidhaa zao tena: \v 12 Bidhaa za dhahabu, za fedha, za vito vya thamani na vya lulu, kitani safi, nguo za rangi ya zambarau, hariri, nguo nyekundu, aina zote za miti ya udi, na vifaa vyote vya pembe za ndovu, vifaa vyote vya miti yenye thamani kuliko yote, shaba, chuma na marumaru, \v 13 bidhaa za mdalasini na vikolezo, za uvumba, manemane, na uvumba wenye harufu nzuri, za divai, na mafuta ya zeituni, za unga mzuri na ngano; ng’ombe na kondoo; farasi na magari ya vita; na miili na roho za wanadamu. \p \v 14 “Watasema, ‘Yale matunda ambayo roho yako iliyatamani yamekoma. Utajiri wako wote na fahari yako vimetoweka, wala haviwezi kupatikana tena kamwe!’ \v 15 Wale wafanyabiashara waliotajirika kwa bidhaa hizo kutoka kwake watasimama mbali naye kwa hofu kubwa ya mateso yanayompata. Watalia na kuomboleza, \v 16 wakisema: \q1 “ ‘Ole! Ole, ee mji mkuu, \q2 uliyekuwa umevikwa mavazi ya kitani safi, \q2 ya rangi ya zambarau na nyekundu, \q1 ukimetameta kwa dhahabu, \q2 vito vya thamani na lulu! \q1 \v 17 Katika muda wa saa moja utajiri wote mkubwa \q2 kama huu umeangamia!’ \p “Kila nahodha, na wote wasafirio kwa meli, na wote wapatao kipato chao kutokana na bahari, watasimama mbali. \v 18 Watakapouona moshi wa kuungua kwake watalia wakisema, ‘Je, kulipata kuwako mji mkubwa kama huu?’ \v 19 Nao watajirushia mavumbi vichwani mwao, huku wakilia na kuomboleza, wakisema: \q1 “ ‘Ole! Ole, ee mji mkubwa, \q2 mji ambao wote wenye meli baharini \q2 walitajirika kupitia kwa mali yake! \q1 Katika saa moja tu ameangamizwa!’ \b \q1 \v 20 “Furahia kwa ajili yake, ee mbingu! \q2 Furahini watakatifu, mitume na manabii! \q1 Mungu amemhukumu \q2 kwa vile alivyowatendea ninyi.” \p \v 21 Kisha malaika mmoja mwenye nguvu akainua jiwe kubwa kama la kusagia, akalitupa baharini akisema: \q1 “Hivyo ndivyo mji mkubwa Babeli \q2 utakavyotupwa chini kwa nguvu, \q2 wala hautaonekana tena. \q1 \v 22 Nyimbo za wapiga vinubi na waimbaji, \q2 wapiga filimbi na wapiga tarumbeta \q2 kamwe hazitasikika tena ndani yako. \q1 Ndani yako kamwe hataonekana tena fundi \q2 mwenye ujuzi wa aina yoyote. \q1 Wala sauti ya jiwe la kusagia \q2 kamwe haitasikika tena. \q1 \v 23 Mwanga wa taa \q2 hautaangaza ndani yako tena. \q1 Sauti ya bwana arusi na bibi arusi \q2 kamwe haitasikika ndani yako tena. \q1 Wafanyabiashara wako walikuwa watu maarufu wa dunia. \q2 Mataifa yote yalipotoshwa kwa uchawi wako. \q1 \v 24 Ndani yake ilionekana damu ya manabii na ya watakatifu, \q2 na wote waliouawa duniani.” \c 19 \s1 Shangwe huko mbinguni \p \v 1 Baada ya haya nikasikia sauti kama ya umati mkubwa mbinguni wakipaza sauti na kusema: \q1 “Haleluya! \q1 Wokovu na utukufu na uweza ni vya Mungu wetu, \q2 \v 2 kwa maana hukumu zake \q2 ni za kweli na za haki. \q1 Amemhukumu yule kahaba mkuu \q2 aliyeuharibu ulimwengu kwa uzinzi wake. \q1 Mungu amemlipiza kisasi \q2 kwa ajili ya damu ya watumishi wake.” \p \v 3 Wakasema tena kwa sauti kuu: \q1 “Haleluya! \q1 Moshi wake huyo kahaba unapanda juu \q2 milele na milele.” \p \v 4 Wale wazee ishirini na wanne pamoja na wale viumbe wanne wenye uhai wakaanguka kifudifudi, wakamwabudu Mungu, aliyekuwa ameketi kwenye kile kiti cha enzi. Wakasema kwa sauti kuu: \q1 “Amen, Haleluya!” \p \v 5 Kisha sauti ikatoka katika kile kiti cha enzi, ikisema: \q1 “Msifuni Mungu wetu, \q2 ninyi watumishi wake wote, \q1 ninyi nyote mnaomcha, \q2 wadogo kwa wakubwa!” \p \v 6 Kisha nikasikia sauti kama ya umati mkubwa, kama sauti ya maji mengi yaendayo kasi na kama ngurumo kubwa ya radi wakipaza sauti na kusema: \q1 “Haleluya! \q2 Kwa maana Bwana Mungu wetu Mwenyezi anatawala. \q1 \v 7 Tufurahi, tushangilie \q2 na kumpa utukufu! \q1 Kwa maana arusi ya Mwana-Kondoo imewadia \q2 na bibi arusi wake amejiweka tayari. \q1 \v 8 Akapewa kitani safi, \q2 inayong’aa na nzuri, \q2 ili avae.” \m (Hiyo kitani safi inawakilisha matendo ya haki ya watakatifu.) \b \p \v 9 Ndipo malaika akaniambia, “Andika: ‘Wamebarikiwa wale walioalikwa kwenye karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo!’ ” Naye akaongeza kusema, “Haya ndio maneno ya kweli ya Mungu.” \p \v 10 Ndipo nikaanguka kifudifudi miguuni pake ili kumwabudu, lakini yeye akaniambia, “Usifanye hivyo! Mimi pia ni mtumishi mwenzako pamoja na ndugu zako walio na ushuhuda wa Isa. Mwabudu Mungu! Maana ushuhuda wa Isa ndio roho ya unabii.” \s1 Aliyepanda farasi mweupe \p \v 11 Kisha nikaona mbingu imefunguka na hapo mbele yangu akiwepo farasi mweupe, ambaye yeye aliyempanda aliitwa Mwaminifu na Kweli. Yeye huhukumu kwa haki na kufanya vita. \v 12 Macho yake ni kama miali ya moto na juu ya kichwa chake kuna taji nyingi. Ana jina lililoandikwa ambalo hakuna mtu yeyote anayelijua isipokuwa yeye mwenyewe. \v 13 Amevaa joho lililoloweshwa katika damu, na Jina lake ni Neno la Mungu. \v 14 Majeshi ya mbinguni walikuwa wakimfuata, wakiwa wamepanda farasi weupe, hali wamevaa mavazi ya kitani safi, nyeupe na nzuri. \v 15 Kinywani mwake hutoka upanga mkali ambao kwa huo atayaangusha mataifa. “Atayatawala kwa fimbo yake ya utawala ya chuma.” Hulikanyaga shinikizo la ghadhabu ya Mungu Mwenyezi. \v 16 Kwenye joho lake na paja lake pameandikwa jina hili: \pc \sc Mfalme wa wafalme\sc* \pc \sc na Bwana wa mabwana.\sc* \s1 Mnyama na majeshi yake washindwa \p \v 17 Nami nikamwona malaika amesimama ndani kwenye jua, naye akaita ndege wote warukao angani kwa sauti kuu, “Njooni, kusanyikeni kwa ajili ya karamu kubwa ya Mungu, \v 18 ili mpate kula nyama ya wafalme na ya majemadari, ya mashujaa, ya farasi na ya wapanda farasi, nyama ya wanadamu, wote walio huru na watumwa, wadogo kwa wakubwa.” \p \v 19 Kisha nikamwona yule mnyama na wafalme wa dunia pamoja na majeshi yao wakiwa wamekusanyika pamoja ili kufanya vita dhidi ya yule aliyempanda farasi pamoja na jeshi lake. \v 20 Lakini yule mnyama akakamatwa pamoja na huyo nabii wa uongo aliyekuwa amefanya ishara kwa niaba ya huyo mnyama, ambaye kwa ishara hizi aliwadanganya wale waliopokea chapa ya huyo mnyama na kuiabudu sanamu yake. Hawa wawili wakatupwa wakiwa hai ndani ya ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti. \v 21 Wale waliosalia waliuawa kwa upanga uliotoka kinywani mwa yule aliyekuwa amempanda farasi nao ndege wote wakajishibisha kwa nyama yao. \c 20 \s1 Utawala wa miaka elfu \p \v 1 Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, akiwa ameshika ufunguo wa lile Shimo na mnyororo mkubwa mkononi mwake. \v 2 Akalishika lile joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni ibilisi, au Shetani, naye akamfunga kwa muda wa miaka elfu. \v 3 Akamtupa katika lile Shimo, akamfunga humo na kulitia muhuri, ili kumzuia asiendelee kudanganya mataifa hadi hiyo miaka elfu itimie. Baada ya hayo lazima afunguliwe kwa muda mfupi. \p \v 4 Kisha nikaona viti vya utawala vilivyokuwa vimekaliwa na wale waliopewa mamlaka ya kuhukumu. Tena nikaona roho za wale waliokatwa vichwa kwa sababu ya ushuhuda wa Isa na kwa sababu ya neno la Mungu. Hawakuwa wamemsujudu huyo mnyama wala sanamu yake wala hawakupokea ile chapa yake kwenye paji za nyuso zao au kwenye mikono yao. Wakawa hai na kutawala pamoja na Al-Masihi miaka elfu. \v 5 (Wafu waliosalia hawakufufuka hadi ilipotimia hiyo miaka elfu.) Huu ndio ufufuo wa kwanza. \v 6 Waliobarikiwa na walio watakatifu ni wale walio na sehemu katika ufufuo wa kwanza. Hao mauti ya pili haina nguvu juu yao, bali watakuwa makuhani wa Mungu na wa Al-Masihi, nao watatawala pamoja naye kwa muda wa miaka elfu. \s1 Shetani ahukumiwa \p \v 7 Hiyo miaka elfu itakapotimia, Shetani atafunguliwa atoke kifungoni mwake, \v 8 naye atatoka ili kuyadanganya mataifa yaliyopo katika pembe nne za dunia, yaani Gogu na Magogu apate kuwakusanya tayari kwa vita. Idadi yao ni kama mchanga ulioko pwani. \v 9 Nao walitembea katika eneo lote la dunia, wakaizunguka kambi ya watakatifu na ule mji unaopendwa. Lakini moto ukashuka kutoka mbinguni na kuwateketeza. \v 10 Naye ibilisi aliyewadanganya akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti walikokuwa wametupwa yule mnyama na yule nabii wa uongo. Watateswa humo usiku na mchana, milele na milele. \s1 Wafu wahukumiwa \p \v 11 Kisha nikaona kiti kikubwa cheupe cha enzi pamoja na yeye aliyeketi juu yake. Dunia na mbingu zikaukimbia uso wake wala mahali pao hapakuonekana. \v 12 Nami nikawaona wafu, wakubwa na wadogo, wakiwa wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi na vitabu vikafunguliwa. Pia kitabu kingine kikafunguliwa ambacho ni kitabu cha uzima. Hao wafu wakahukumiwa sawasawa na matendo yao kama yalivyoandikwa ndani ya hivyo vitabu. \v 13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo, nayo mauti na Kuzimu\f + \fr 20:13 \fr*\ft Kuzimu kwa Kiyunani ni \ft*\fqa Hades\fqa*\ft , yaani \ft*\fqa mahali pa wafu.\fqa*\f* zikawatoa wafu waliokuwamo. Kila mtu akahukumiwa kulingana na yale aliyoyatenda. \v 14 Kisha mauti na Kuzimu zikatupwa katika ziwa la moto. Hii ndio mauti ya pili, yaani hilo ziwa la moto. \v 15 Iwapo mtu yeyote jina lake halikuonekana katika kile kitabu cha uzima, alitupwa ndani ya lile ziwa la moto. \c 21 \s1 Mbingu mpya na nchi mpya \p \v 1 Kisha nikaona “mbingu mpya na nchi mpya”, kwa maana mbingu ya kwanza na nchi ya kwanza vimekwisha kupita, wala hapakuwa na bahari tena. \v 2 Nikauona Mji Mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, ukiwa umeandaliwa kama bibi arusi aliyepambwa kwa ajili ya mumewe. \v 3 Nami nikasikia sauti kubwa kutoka kile kiti cha enzi ikisema, “Sasa makao ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atakaa pamoja nao. Yeye atakuwa Mungu wao nao watakuwa watu wake, naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. \v 4 Atafuta kila chozi kutoka macho yao. Mauti haitakuwepo tena, wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu, kwa maana mambo ya kwanza yamekwisha kupita.” \p \v 5 Naye yule aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi akasema, “Tazama, nayafanya mambo yote kuwa mapya!” Kisha akasema, “Andika haya, maana maneno haya ni ya kuaminika tena ni kweli.” \p \v 6 Akaniambia, “Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Yeye aonaye kiu nitampa kunywa kutoka chemchemi ya maji ya uzima bila gharama yoyote. \v 7 Yeye ashindaye atayarithi haya yote, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu. \v 8 Lakini waoga, wasioamini, wachafu, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, pamoja na waongo wote, mahali pao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.” \p \v 9 Mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na yale mabakuli saba ya hayo mapigo saba ya mwisho akaja akaniambia, “Njoo, nami nitakuonesha bibi arusi, yaani mke wa Mwana-Kondoo.” \v 10 Naye akanichukua katika Roho wa Mungu hadi kwenye mlima mkubwa na mrefu, akanionesha ule Mji Mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu. \v 11 Ulikuwa uking’aa kwa utukufu wa Mungu kama kito chenye thamani sana, kama yaspi, safi kama kioo. \v 12 Ulikuwa na ukuta mkubwa, mrefu wenye malango kumi na mawili, pakiwa na malaika kumi na wawili kwenye hayo malango. Kwenye malango hayo yaliandikwa majina ya yale makabila kumi na mawili ya Israeli. \v 13 Kulikuwa na malango matatu upande wa mashariki, matatu upande wa kaskazini, matatu upande wa kusini na matatu upande wa magharibi. \v 14 Ukuta wa huo mji ulikuwa na misingi kumi na mbili, na juu yake yaliandikwa majina ya wale mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo. \p \v 15 Huyo malaika aliyesema nami alikuwa na ufito wa dhahabu wa kupimia huo mji, malango yake na kuta zake. \v 16 Mji huo ulikuwa mraba, urefu wake ulikuwa sawa na upana wake. Akaupima huo mji kwa huo ufito akakuta una kama stadioni 12,000\f + \fr 21:16 \fr*\ft ni kama kilomita 2,200\ft*\f*; urefu wake na upana wake na kwenda juu kwake vilikuwa sawa. \v 17 Akaupima ukuta wake, ulikuwa na unene wa dhiraa mia moja na arobaini na nne (144)\f + \fr 21:17 \fr*\ft ni karibu mita sitini na tano\ft*\f* kwa kipimo cha kibinadamu ambacho huyo malaika alikuwa akikitumia. \v 18 Ukuta huo ulijengwa kwa yaspi hali mji wenyewe ulijengwa kwa dhahabu safi, iking’aa kama kioo. \v 19 Misingi ya kuta za mji huo zilipambwa kwa kila aina ya kito cha thamani. Msingi wa kwanza ulikuwa wa yaspi, wa pili yakuti samawi, wa tatu kalkedoni, wa nne zumaridi, \v 20 wa tano sardoniki, wa sita akiki, wa saba krisolitho, wa nane zabarajadi, wa tisa yakuti manjano, wa kumi krisopraso, wa kumi na moja hiakintho, wa kumi na mbili amethisto. \v 21 Yale malango kumi na mbili yalikuwa ni lulu kumi na mbili, kila lango lilikuwa limetengenezwa kwa lulu moja. Barabara kuu ya mji huo ilikuwa ya dhahabu safi iliyong’aa kama kioo. \p \v 22 Sikuona Hekalu ndani ya huo mji kwa sababu Bwana Mungu Mwenyezi na Mwana-Kondoo ndio Hekalu lake. \v 23 Ule mji hauhitaji jua wala mwezi kuuangazia, kwa sababu utukufu wa Mungu ndio nuru yake na Mwana-Kondoo ndiye taa yake. \v 24 Mataifa yatatembea yakiangaziwa na nuru yake na wafalme wa duniani wataleta fahari yao ndani yake. \v 25 Malango yake hayatafungwa kamwe, kwa maana hakutakuwa na usiku humo. \v 26 Utukufu na heshima za mataifa zitaletwa humo. \v 27 Lakini kitu kichafu hakitaingia humo kamwe, wala mtu yeyote atendaye mambo ya aibu au ya udanganyifu. Bali watakaoingia humo ni wale tu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo. \c 22 \s1 Mto wa maji ya uzima \p \v 1 Kisha yule malaika akanionesha mto wa maji ya uzima, maangavu kama kioo yakitiririka kutoka kwa kile kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo, \v 2 kupitia katikati ya barabara kuu ya huo mji. Kwenye kila upande wa huo mto kulikuwa na mti wa uzima utoao matunda ya aina kumi na mbili, ukizaa matunda yake kila mwezi. Nayo majani ya mti huo ni kwa ajili ya uponyaji wa mataifa. \v 3 Katika mji huo hakutakuwa tena na laana, bali kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kitakuwamo humo na watumishi wake watamtumikia, \v 4 nao watamwona uso wake na Jina lake litakuwa kwenye paji za nyuso zao. \v 5 Usiku hautakuwako tena, wala hawatahitaji mwanga wa taa au wa jua, kwa maana Bwana Mwenyezi Mungu atakuwa nuru yao, nao watatawala milele na milele. \p \v 6 Kisha yule malaika akaniambia, “Maneno haya ni ya kuaminika na kweli. Mwenyezi Mungu, Mungu wa roho za manabii, alimtuma malaika wake kuwaonesha watumishi wake yale ambayo hayana budi kutukia upesi.” \b \s1 Bwana Isa anakuja \p \v 7 “Tazama, naja upesi! Amebarikiwa yeye ayashikaye maneno ya unabii wa kitabu hiki.” \b \p \v 8 Mimi, Yohana, ndiye niliyesikia na kuyaona mambo haya. Nilipokwisha kuyasikia na kuyaona, nilianguka chini nikasujudu miguuni pa yule malaika aliyekuwa akinionesha mambo hayo. \v 9 Lakini yeye akaniambia, “Usifanye hivyo! Mimi ni mtumishi pamoja nawe na ndugu zako manabii na wote wanaoyashika maneno ya kitabu hiki. Msujudie Mungu!” \p \v 10 Kisha akaniambia, “Usiyafunge maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, kwa sababu wakati umekaribia. \v 11 Atendaye mabaya na aendelee kutenda mabaya, aliye mchafu na aendelee kuwa mchafu, yeye atendaye haki na aendelee kutenda haki, na yeye aliye mtakatifu na aendelee kuwa mtakatifu.” \b \p \v 12 “Tazama, naja upesi! Thawabu yangu i mkononi mwangu, nami nitampa kila mtu sawasawa na alivyotenda. \v 13 Mimi ni Alfa na Omega, wa Kwanza na wa Mwisho, Mwanzo na Mwisho. \b \p \v 14 “Wamebarikiwa wale wafuao mavazi yao, ili wapate haki ya kuuendea huo mti wa uzima na kuuingia huo mji kupitia kwenye malango yake. \v 15 Huko nje wako mbwa, wachawi, wazinzi, wauaji, waabudu sanamu, na kila mtu apendaye udanganyifu na kuufanya. \b \p \v 16 “Mimi, Isa, nimemtuma malaika wangu kushuhudia mambo haya kwa ajili ya jumuiya ya waumini. Mimi ndimi Shina na Mzao wa Daudi, ile Nyota ya Asubuhi inayong’aa.” \b \p \v 17 Roho wa Mungu na bibi arusi wanasema, “Njoo!” Naye asikiaye na aseme, “Njoo!” Yeyote mwenye kiu na aje, na kila anayetaka na anywe maji ya uzima bure. \b \p \v 18 Namwonya kila mtu asikiaye maneno ya unabii wa kitabu hiki: Mtu yeyote akiongeza humo chochote, Mungu atamwongezea mapigo yaliyoandikwa katika kitabu hiki. \v 19 Kama mtu yeyote akipunguza humo chochote katika maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mungu atamwondolea sehemu yake katika ule mti wa uzima na katika ule Mji Mtakatifu, ambao habari zake zimeandikwa katika kitabu hiki. \b \p \v 20 Yeye anayeshuhudia mambo haya asema, “Hakika, naja upesi!” \p Amen. Njoo, Bwana Isa. \b \p \v 21 Neema ya Bwana Isa iwe na watakatifu wote. Amen.