\id 1CO - Biblica® Open Kiswahili Contemporary Scriptures (Biblica® Toleo Wazi Neno: Maandiko Matakatifu) \usfm 3.0 \ide UTF-8 \h 1 Wakorintho \toc1 1 Wakorintho \toc2 1 Wakorintho \toc3 1Kor \mt1 1 Wakorintho \c 1 \s1 Salamu \po \v 1 Paulo, niliyeitwa kwa mapenzi ya Mungu kuwa mtume wa Al-Masihi Isa, na Sosthene ndugu yetu. \po \v 2 Kwa kundi la waumini wa Mungu walioko Korintho, kwa wale waliotakaswa katika Al-Masihi Isa na walioitwa kuwa watakatifu, pamoja na wale wote ambao kila mahali wanaliitia Jina la Al-Masihi Isa Bwana wetu, aliye Bwana wao na wetu pia. \po \v 3 Neema na amani zinazotoka kwa Mungu, Baba\f + \fr 1:3 \fr*\ft Kwa mwanadamu, Mwenyezi Mungu ni Baba kupitia uhusiano unaopatikana katika kumtumaini Isa Al-Masihi.\ft*\f* yetu, na kwa Bwana wetu Isa Al-Masihi ziwe nanyi. \s1 Shukrani \p \v 4 Ninamshukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu kwa sababu ya neema yake mliyopewa katika Al-Masihi Isa. \v 5 Kwa kuwa katika Al-Masihi mmetajirishwa kwa kila hali, katika kusema kwenu na katika maarifa yenu yote, \v 6 kwa sababu ushuhuda wetu kumhusu Al-Masihi ulithibitishwa ndani yenu. \v 7 Kwa hiyo hamkupungukiwa na karama yoyote ya kiroho wakati mnangoja kwa shauku kudhihirishwa kwa Bwana wetu Isa Al-Masihi. \v 8 Atawafanya imara hadi mwisho, ili msiwe na hatia siku ile ya Bwana wetu Isa Al-Masihi. \v 9 Mungu ambaye mmeitwa naye ili mwe na ushirika na Mwanawe Isa Al-Masihi, Bwana wetu ni mwaminifu. \s1 Mgawanyiko katika kundi la waumini \p \v 10 Nawasihi ndugu zangu, katika Jina la Bwana wetu Isa Al-Masihi, kwamba mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi, ili pasiwepo na matengano kati yenu, na kwamba mwe na umoja kikamilifu katika nia na katika kusudi. \v 11 Ndugu zangu, nimepata habari kutoka kwa baadhi ya watu wa nyumbani mwa Kloe kwamba kuna magomvi kati yenu. \v 12 Maana yangu ni kwamba: Mmoja wenu husema, “Mimi ni wa Paulo”; mwingine, “Mimi ni wa Apolo”; mwingine, “Mimi ni wa Kefa\f + \fr 1:12 \fr*\ft yaani \ft*\fqa Petro\fqa*\f*”; na mwingine, “Mimi ni wa Al-Masihi.” \p \v 13 Je, Al-Masihi amegawanyika? Je, Paulo ndiye alisulubishwa kwa ajili yenu? Je, mlibatizwa\f + \fr 1:13 \fr*\ft Ubatizo ni ishara ya kuungama dhambi na kusamehewa na Mwenyezi Mungu, na kuweka nadhiri ya kubadilisha mienendo ya awali. Wafuasi wa Isa Al-Masihi pia wanapokea Roho wa Mungu kama dhibitisho ya imani yao.\ft*\f* kwa jina la Paulo? \v 14 Nashukuru kwamba sikumbatiza mtu yeyote isipokuwa Krispo na Gayo. \v 15 Kwa hiyo hakuna mtu yeyote anayeweza kusema kwamba alibatizwa kwa jina langu. \v 16 (Naam, niliwabatiza pia watu wa nyumbani mwa Stefana; lakini zaidi ya hao sijui kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.) \v 17 Kwa maana Al-Masihi hakunituma ili kubatiza bali kuhubiri Injili; sio kwa maneno ya hekima ya kibinadamu, ili msalaba wa Al-Masihi usije ukakosa nguvu yake. \s1 Al-Masihi ni hekima na nguvu ya Mwenyezi Mungu \p \v 18 Kwa maana ujumbe wa msalaba kwa wale wanaopotea ni upuzi, lakini kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu. \v 19 Kwa maana imeandikwa: \q1 “Nitaiharibu hekima ya wenye hekima, \q2 na kubatilisha akili ya wenye akili.” \p \v 20 Yuko wapi mwenye hekima? Yuko wapi msomi? Yuko wapi mwanafalsafa wa nyakati hizi? Je, Mungu hakufanya hekima ya ulimwengu huu kuwa upumbavu? \v 21 Kwa kuwa katika hekima ya Mungu ulimwengu kwa hekima yake haukumjua yeye, ilimpendeza Mungu kuwaokoa walioamini kwa upuzi wa lile neno lililohubiriwa. \v 22 Wayahudi wanadai ishara za miujiza na Wayunani wanatafuta hekima. \v 23 Lakini sisi tunamhubiri Al-Masihi aliyesulubiwa: yeye kwa Wayahudi ni kikwazo na kwa Wayunani ni upuzi. \v 24 Lakini kwa wale ambao Mungu amewaita, Wayahudi na pia Wayunani, Al-Masihi ndiye nguvu ya Mungu na pia hekima ya Mungu. \v 25 Kwa maana upumbavu wa Mungu una hekima zaidi ya hekima ya wanadamu, nao udhaifu wa Mungu una nguvu kuliko nguvu ya wanadamu. \p \v 26 Ndugu zangu, kumbukeni mlivyokuwa mlipoitwa. Kwa kipimo cha kibinadamu, si wengi wenu mliokuwa na hekima. Si wengi mliokuwa na ushawishi, si wengi mliozaliwa katika vyeo. \v 27 Lakini Mungu alivichagua vitu vipumbavu vya ulimwengu ili awaaibishe wenye hekima; Mungu alivichagua vitu dhaifu vya ulimwengu ili awaaibishe wenye nguvu. \v 28 Alivichagua vitu vya chini na vinavyodharauliwa vya dunia hii, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko, \v 29 ili mtu yeyote asijisifu mbele zake. \v 30 Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Al-Masihi Isa, aliyefanyika kwetu hekima inayotoka kwa Mungu, yaani haki yetu, na utakatifu na ukombozi. \v 31 Hivyo, kama ilivyoandikwa: “Yeye ajisifuye na ajisifu katika Mwenyezi Mungu.” \c 2 \s1 Kumtangaza Al-Masihi aliyesulubiwa \p \v 1 Ndugu zangu nilipokuja kwenu, sikuja na maneno ya ushawishi wala hekima ya hali ya juu nilipowahubiria siri ya Mungu. \v 2 Kwa kuwa niliamua kutokujua kitu chochote nilipokuwa nanyi, isipokuwa Isa Al-Masihi aliyesulubiwa. \v 3 Mimi nilikuja kwenu nikiwa dhaifu na mwenye hofu na kwa kutetemeka sana. \v 4 Kuhubiri kwangu na ujumbe wangu haukuwa kwa hekima na maneno ya ushawishi, bali kwa madhihirisho ya nguvu za Roho wa Mungu, \v 5 ili imani yenu isiwe imejengwa katika hekima ya wanadamu bali katika nguvu za Mungu. \s1 Hekima ya kweli itokayo kwa Mwenyezi Mungu \p \v 6 Lakini miongoni mwa watu waliokomaa twanena hekima, wala si hekima ya ulimwengu huu au ya watawala wa dunia hii wanaobatilika. \v 7 Sisi tunanena hekima ya Mungu ambayo ni siri, tena iliyofichika, ambayo Mungu aliikusudia kabla ya ulimwengu kuumbwa, kwa ajili ya utukufu wetu. \v 8 Hakuna hata mtawala mmoja wa nyakati hizi aliyeelewa jambo hili. Kwa maana kama wangeelewa, hawangemsulubisha Bwana wa utukufu. \v 9 Lakini ni kama ilivyoandikwa: \q1 “Hakuna jicho limepata kuona, \q2 wala sikio limepata kusikia, \q1 wala hayakuingia moyoni mwa mwanadamu yeyote, \q2 mambo ambayo Mungu amewaandalia \q2 wale wanaompenda”: \m \v 10 Lakini mambo haya Mungu ametufunulia kwa Roho wake. \p Roho huchunguza kila kitu, hata mambo ya ndani sana ya Mungu. \v 11 Kwa maana ni nani anayejua mawazo ya mtu isipokuwa roho iliyo ndani ya huyo mtu? Vivyo hivyo hakuna mtu ajuaye mawazo ya Mungu isipokuwa Roho Mtakatifu wa Mungu. \v 12 Basi hatukupokea roho ya dunia bali Roho atokaye kwa Mungu, ili tuweze kuelewa kile kipawa ambacho Mungu ametupatia bure. \v 13 Haya ndio tusemayo, si kwa maneno tuliyofundishwa kwa hekima ya wanadamu bali kwa maneno tuliyofundishwa na Roho, tukifafanua kweli za kiroho kwa maneno ya kiroho. \v 14 Mtu ambaye hana Roho hawezi kupokea mambo yanayotoka kwa Roho wa Mungu, kwa kuwa ni upuzi kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa sababu hayo yanaeleweka tu kwa upambanuzi wa rohoni. \v 15 Mtu wa kiroho hubainisha mambo yote, lakini yeye mwenyewe habainishwi na mtu yeyote. \q1 \v 16 “Kwa maana ni nani aliyefahamu mawazo ya Mwenyezi Mungu \q2 ili apate kumfundisha?” \m Lakini sisi tunayo mawazo ya Al-Masihi. \c 3 \s1 Kuhusu mgawanyiko katika kundi la waumini \p \v 1 Ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu wa kiroho, bali kama watu wa mwilini, kama watoto wachanga katika Al-Masihi. \v 2 Niliwanywesha maziwa, wala si chakula kigumu, kwa kuwa hamkuwa tayari kwa hicho chakula. Naam, hata sasa hamko tayari. \v 3 Ninyi bado ni watu wa mwilini. Kwa kuwa bado kuna wivu na magombano miongoni mwenu, je, ninyi si watu wa mwilini? Je, si mwaendelea kama watu wa kawaida? \v 4 Kwa maana mmoja anaposema, “Mimi ni wa Paulo,” na mwingine, “Mimi ni wa Apolo,” je, ninyi si wanadamu wa kawaida? \p \v 5 Kwani, Apolo ni nani? Naye Paulo ni nani? Ni watumishi tu ambao kupitia wao mliamini, kama vile Bwana Isa alivyompa kila mtu huduma yake. \v 6 Mimi nilipanda mbegu, Apolo akatia maji, lakini Mungu ndiye aliikuza. \v 7 Hivyo mwenye kupanda na mwenye kutia maji si kitu, bali Mungu peke yake ambaye huifanya ikue. \v 8 Apandaye mbegu ana lengo sawa na yule atiaye maji na kila mmoja atalipwa kulingana na kazi yake. \v 9 Kwa kuwa sisi tu watendakazi pamoja na Mungu. Ninyi ni shamba la Mungu, jengo la Mungu. \p \v 10 Kwa neema Mungu aliyonipa, niliweka msingi kama mjenzi stadi na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mmoja inampasa awe mwangalifu jinsi anavyojenga. \v 11 Kwa maana hakuna mtu yeyote awezaye kuweka msingi mwingine wowote isipokuwa ule uliokwisha kuwekwa, ambao ni Isa Al-Masihi. \v 12 Kama mtu yeyote akijenga juu ya msingi huu kwa kutumia dhahabu, fedha, vito vya thamani, miti, majani au nyasi, \v 13 kazi yake itaonekana ilivyo, kwa kuwa Siku ile itaidhihirisha. Itadhihirishwa kwa moto, nao moto utapima ubora wa kazi ya kila mtu. \v 14 Kama kile alichojenga kitabaki, atapokea thawabu yake. \v 15 Kama kitateketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa, lakini tu kama mtu aliyenusurika kwenye moto. \p \v 16 Je, hamjui kwamba ninyi wenyewe ni hekalu la Mungu na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu? \v 17 Kama mtu yeyote akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamwangamiza; kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, na ninyi ndio hilo hekalu. \p \v 18 Msijidanganye. Kama mtu yeyote miongoni mwenu akidhani kuwa ana hekima kwa viwango vya dunia hii, inampasa awe mjinga ili apate kuwa na hekima. \v 19 Kwa maana hekima ya ulimwengu huu ni upuzi mbele za Mungu. Kama ilivyoandikwa: “Mungu huwanasa wenye hekima katika hila yao,” \v 20 tena, “Mwenyezi Mungu anajua kwamba mawazo ya wenye hekima ni ubatili.” \v 21 Hivyo basi, mtu asijivune kuhusu wanadamu! Vitu vyote ni vyenu, \v 22 iwe ni Paulo au Apolo au Kefa\f + \fr 3:22 \fr*\ft yaani \ft*\fqa Petro\fqa*\f*, au dunia au uzima au mauti, au wakati uliopo au ujao: haya yote ni yenu, \v 23 na ninyi ni wa Al-Masihi, naye Al-Masihi ni wa Mungu. \c 4 \s1 Mawakili wa siri za Mwenyezi Mungu \p \v 1 Basi, watu na watuhesabu sisi kuwa tu watumishi wa Al-Masihi na mawakili wa siri za Mungu. \v 2 Tena, litakiwalo ni mawakili waonekane kuwa waaminifu. \v 3 Lakini kwangu mimi ni jambo dogo sana kwamba nihukumiwe na ninyi au na mahakama yoyote ya kibinadamu. Naam, hata mimi mwenyewe sijihukumu. \v 4 Dhamiri yangu ni safi, lakini hilo halinihesabii kuwa asiye na hatia. Bwana Isa ndiye anihukumuye. \v 5 Kwa hiyo msihukumu jambo lolote kabla ya wakati wake. Ngojeni hadi Bwana Isa atakapokuja. Yeye atayaleta nuruni mambo yale yaliyofichwa gizani, na kuweka wazi nia za mioyo ya wanadamu. Wakati huo kila mmoja atapokea sifa anayostahili kutoka kwa Mungu. \p \v 6 Basi ndugu zangu, mambo haya nimeyafanya kwangu binafsi na Apolo kwa faida yenu, ili mweze kujifunza kutoka kwetu maana ya ule usemi usemao, “Msivuke zaidi ya yale yaliyoandikwa.” Hivyo hamtajivunia mtu fulani na kumdharau mwingine. \v 7 Kwa maana ni nani aliyewafanya kuwa tofauti na wengine? Ni nini mlicho nacho ambacho hamkupokea? Nanyi kama mlipokea, kwa nini mnajivuna kama vile hamkupokea? \p \v 8 Sasa tayari mnayo yale yote mnayohitaji! Tayari mmekwisha kuwa matajiri! Mmekuwa wafalme, tena bila sisi! Laiti mngekuwa wafalme kweli ili na sisi tupate kuwa wafalme pamoja nanyi! \v 9 Kwa maana ninaona kwamba Mungu ametuweka sisi mitume katika nafasi ya mwisho kabisa, kama watu waliohukumiwa kufa kwenye uwanja wa tamasha, kwa sababu tumefanywa kuwa maonesho kwa ulimwengu wote, kwa malaika na kwa wanadamu pia. \v 10 Kwa ajili ya Al-Masihi sisi ni wajinga, lakini ninyi mna hekima sana ndani ya Al-Masihi. Sisi tu dhaifu, lakini ninyi mna nguvu. Tunadharauliwa, lakini ninyi mnaheshimiwa. \v 11 Hadi saa hii tuna njaa na kiu, tu uchi, tumepigwa na hatuna makao. \v 12 Tunafanya kazi kwa bidii kwa mikono yetu wenyewe. Tunapolaaniwa, tunabariki; tunapoteswa, tunastahimili; \v 13 tunaposingiziwa, tunajibu kwa upole. Hadi sasa tumekuwa kama takataka ya dunia na uchafu wa ulimwengu. \p \v 14 Siwaandikii mambo haya ili kuwaaibisha, bali ili kuwaonya, kama wanangu wapendwa. \v 15 Hata kama mnao walimu elfu kumi katika Al-Masihi, lakini hamna baba wengi. Mimi nilikuwa baba yenu katika Al-Masihi Isa kwa kuwaletea Injili. \v 16 Basi nawasihi igeni mfano wangu. \v 17 Kwa sababu hii ninamtuma Timotheo, mwanangu mpendwa na mwaminifu katika Bwana Isa. Yeye atawakumbusha kuhusu njia za maisha yangu katika Al-Masihi Isa, ambayo yanakubaliana na mafundisho yangu ninayofundisha katika kila kundi la waumini. \p \v 18 Baadhi yenu mmekuwa na jeuri mkidhani kuwa sitafika kwenu. \v 19 Lakini kama Bwana Isa akipenda, nitafika kwenu hivi karibuni, nami nitajua, si tu kile wanachosema hawa watu jeuri, bali pia nguvu yao. \v 20 Kwa kuwa ufalme wa Mungu si maneno matupu tu bali ni nguvu. \v 21 Ninyi amueni. Je, nije kwenu na fimbo, au nije kwa upendo na kwa roho ya upole? \c 5 \s1 Mwasherati atengwe \p \v 1 Yamkini habari imeenea ya kuwa miongoni mwenu kuna uzinzi ambao haujafanyika hata miongoni mwa watu wasiomjua Mungu: Kwamba mtu anaishi na mke wa baba yake. \v 2 Nanyi mwajivuna! Je, haiwapasi kuhuzunika na kumtenga na ushirika wenu mtu huyo aliyefanya mambo hayo? \v 3 Hata kama siko pamoja nanyi katika mwili, niko nanyi katika roho. Nami nimekwisha kumhukumu mtu huyo aliyetenda jambo hili, kama vile ningekuwepo. \v 4 Mnapokutana katika Jina la Bwana wetu Isa nami nikiwepo pamoja nanyi katika roho, na uweza wa Bwana Isa ukiwepo, \v 5 mkabidhini mtu huyu kwa Shetani, ili mwili wake uharibiwe, lakini roho yake iokolewe katika siku ya Mwenyezi Mungu. \p \v 6 Majivuno yenu si mazuri. Je, hamjui kwamba chachu kidogo huchachusha donge zima la unga? \v 7 Ondoeni chachu ya kale ili mpate kuwa donge jipya lisilotiwa chachu, kama vile mlivyo. Kwa maana Al-Masihi, Mwana-Kondoo wetu wa Pasaka\f + \fr 5:7 \fr*\ft Sherehe iliyowakumbusha Waisraeli jinsi Mwenyezi Mungu alivyowakomboa kutoka utumwani huko Misri.\ft*\f* amekwisha tolewa kuwa dhabihu. \v 8 Kwa hiyo, tusiiadhimishe sikukuu hii kwa chachu ya zamani, chachu ya nia mbaya na uovu, bali kwa mkate usiotiwa chachu, ndio weupe wa moyo na kweli. \p \v 9 Niliwaandikia katika waraka wangu kuwa msishirikiane na wazinzi. \v 10 Sina maana kwamba msishirikiane na wazinzi wa ulimwengu huu, au wenye tamaa mbaya, wanyang’anyi au waabudu sanamu. Kwa kufanya hivyo ingewalazimu mtoke ulimwenguni humu. \v 11 Lakini sasa nawaandikia kwamba msishirikiane na mtu yeyote anayejiita ndugu, hali akiwa ni mzinzi, au mwenye tamaa mbaya, mwabudu sanamu au msingiziaji, mlevi au mdhalimu. Mtu kama huyo hata msile naye. \p \v 12 Yanihusu nini kuwahukumu wale watu walio nje ya kundi la waumini? Je, si mnapaswa kuwahukumu hao walio ndani? \v 13 Mungu atawahukumu hao walio nje. “Ninyi mwondoeni huyo mtu mwovu miongoni mwenu.” \c 6 \s1 Kushtakiana miongoni mwa waumini \p \v 1 Kama mtu yeyote wa kwenu ana ugomvi na mwenzake, anathubutuje kuupeleka kwa wasiomcha Mungu ili kuamuliwa badala ya kuupeleka kwa watakatifu? \v 2 Je, hamjui kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Nanyi kama mtauhukumu ulimwengu, je, hamwezi kuamua mambo madogo madogo? \v 3 Hamjui kwamba tutawahukumu malaika? Je, si zaidi mambo ya maisha haya? \v 4 Kwa hiyo kama kuna ugomvi miongoni mwenu kuhusu mambo kama haya, je, mnachagua watu ambao wanaonekana hata sio wa heshima katika kundi la waumini kuwa waamuzi kati yenu? \v 5 Nasema hivi ili mwone aibu. Je, inawezekana kuwa miongoni mwenu hakuna mtu mwenye hekima ya kutosha kuamua ugomvi kati ya waumini? \v 6 Badala yake ndugu mmoja anampeleka mwenzake mahakamani, tena mbele ya watu wasioamini! \p \v 7 Huko kuwa na mashtaka miongoni mwenu ina maana kwamba tayari ni kushindwa kabisa. Kwa nini msikubali kutendewa mabaya? Kwa nini msikubali kunyang’anywa? \v 8 Badala yake, ninyi wenyewe mwadanganya na kutenda mabaya, tena mwawatendea ndugu zenu. \p \v 9 Je, hamjui kwamba wasio haki hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike: Waasherati, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wahanithi, wala walawiti, \v 10 wala wezi, wala wenye tamaa mbaya, wala walevi, wala wanaodhihaki, wala wanyang’anyi hawataurithi ufalme wa Mungu. \v 11 Baadhi yenu mlikuwa kama hao. Lakini mlioshwa, mlitakaswa, mlihesabiwa haki kwa jina la Bwana Isa Al-Masihi na katika Roho wa Mungu wetu. \s1 Dhambi za zinaa \p \v 12 “Vitu vyote ni halali kwangu”: lakini si vitu vyote vyenye faida. “Vitu vyote ni halali kwangu”: lakini sitatawaliwa na kitu chochote. \v 13 “Chakula ni cha tumbo, na tumbo ni la chakula”: lakini Mungu ataviangamiza vyote viwili. Mwili sio kwa ajili ya zinaa, bali kwa ajili ya Bwana Isa, na Bwana Isa kwa ajili ya mwili. \v 14 Naye Mungu aliyemfufua Bwana Isa kutoka kwa wafu atatufufua sisi pia kwa uweza wake. \v 15 Je, hamjui kwamba miili yenu ni viungo vya Al-Masihi mwenyewe? Je, nichukue viungo vya mwili wa Al-Masihi na kuviunganisha na mwili wa kahaba? La hasha! \v 16 Hamjui kwamba aliyeungwa na kahaba anakuwa mwili mmoja naye? Kwa kuwa imenenwa, “Hao wawili watakuwa mwili mmoja.” \v 17 Lakini mtu aliyeungwa na Bwana Isa anakuwa roho moja naye. \p \v 18 Ikimbieni zinaa. Dhambi zingine zote atendazo mtu ziko nje ya mwili wake, lakini yeye aziniye hutenda dhambi ndani ya mwili wake mwenyewe. \v 19 Je, hamjui kwamba miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu wa Mungu akaaye ndani yenu, ambaye mmepewa na Mungu? Ninyi si mali yenu wenyewe, \v 20 kwa maana mmenunuliwa kwa gharama. Kwa hiyo mtukuzeni Mungu katika miili yenu. \c 7 \s1 Kuhusu ndoa \p \v 1 Basi kuhusu mambo yale mliyoyaandika: “Ni vyema mwanaume asimguse mwanamke.” \v 2 Lakini ili kuepuka zinaa, kila mwanaume na awe na mke wake mwenyewe na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe. \v 3 Mume atimize wajibu wake wa ndoa kwa mkewe, naye vivyo hivyo mke kwa mumewe. \v 4 Mwanamke hana mamlaka juu ya mwili wake bali mumewe, wala mume hana mamlaka juu ya mwili wake bali mkewe. \v 5 Msinyimane, isipokuwa mmekubaliana kufanya hivyo kwa muda, ili mweze kujitoa kwa maombi. Kisha mrudiane tena, ili Shetani asije akapata nafasi ya kuwajaribu kwa sababu ya kutokuwa na kiasi. \v 6 Nasema haya kama ushauri na si amri. \v 7 Laiti watu wangekuwa kama mimi nilivyo. Lakini kila mtu amepewa kipawa chake kutoka kwa Mungu, mmoja ana kipawa cha namna hii na mwingine ana cha namna ile. \p \v 8 Kwa wale wasiooa na kwa wajane, nasema hivi, ingekuwa vizuri wasioe. \v 9 Lakini kama hawawezi kujizuia, basi waoe na kuolewa, kwa maana ni afadhali kuoa au kuolewa kuliko kuwaka tamaa. \p \v 10 Kwa wale waliooana nawapa amri (si mimi, ila ni Bwana Isa): Mke asitengane na mumewe. \v 11 Lakini akitengana, ni lazima akae bila kuolewa, ama sivyo apatane tena na mumewe. Wala mume asimpe mkewe talaka. \p \v 12 Lakini kwa wengine nasema (si Bwana Isa, ila ni mimi): Kama ndugu ana mke asiyeamini, naye huyo mke anakubali kuishi pamoja naye, basi asimwache. \v 13 Naye mwanamke aaminiye kama ameolewa na mwanaume asiyeamini na huyo mume anakubali kuishi naye, basi huyo mwanamke asimwache. \v 14 Kwa maana huyo mume asiyeamini anatakaswa kupitia mkewe, naye mke asiyeamini anatakaswa kupitia mumewe anayeamini. Kama haingekuwa hivyo watoto wenu wangakuwa si safi; lakini ilivyo sasa, wao ni watakatifu. \p \v 15 Lakini kama yule asiyeamini akijitenga, basi afanye hivyo. Katika hali kama hiyo mwanamke au mwanaume aaminiye hafungwi, kwa sababu Mungu ametuita tuishi kwa amani. \v 16 Wewe mke, unajuaje kama utamwokoa mumeo? Au wewe mume, unajuaje kama utamwokoa mkeo? \s1 Kuishi kama alivyoagiza Bwana Isa \p \v 17 Lakini kila mtu na aishi maisha aliyopangiwa na Bwana Isa, yale Mungu aliyomwitia. Hii ni sheria ninayoiweka kwa makundi yote ya waumini. \v 18 Je, mtu alikuwa tayari ametahiriwa alipoitwa? Asijifanye asiyetahiriwa. Je, mtu alikuwa hajatahiriwa alipoitwa? Asitahiriwe. \v 19 Kutahiriwa si kitu, na kutokutahiriwa si kitu. Lakini kuzitii amri za Mungu ndilo jambo muhimu. \v 20 Basi kila mtu na abaki katika hali aliyoitwa nayo. \p \v 21 Je, wewe ulipoitwa ulikuwa mtumwa? Jambo hilo lisikusumbue. Ingawaje unaweza kupata uhuru, tumia nafasi uliyo nayo sasa kuliko wakati mwingine wowote. \v 22 Kwa maana yeyote aliyeitwa katika Bwana Isa akiwa mtumwa yeye ni mtu huru kwa Bwana Isa, kama vile yeyote aliyekuwa huru alipoitwa yeye ni mtumwa wa Al-Masihi. \v 23 Mlinunuliwa kwa gharama; msiwe watumwa wa wanadamu. \v 24 Ndugu zangu, kama kila mtu alivyoitwa, akae katika wito wake alioitiwa na Mungu. \s1 Wajane na wasioolewa \p \v 25 Basi, kuhusu wale walio bikira, mimi sina amri kutoka kwa Bwana Isa, lakini mimi natoa shauri kama mtu ambaye ni mwaminifu kwa rehema za Bwana Isa. \v 26 Kwa sababu ya shida iliyopo sasa, naona ni vyema mkibaki kama mlivyo. \v 27 Je, umeolewa? Basi usitake talaka. Je, hujaoa? Usitafute mke. \v 28 Lakini kama ukioa, hujatenda dhambi; na kama bikira akiolewa, hajatenda dhambi. Lakini wale wanaooa watakabiliana na matatizo mengi katika maisha haya, nami nataka kuwazuilia hayo. \p \v 29 Lakini ndugu zangu, nina maana kwamba muda uliobaki ni mfupi. Tangu sasa wale waliooa waishi kama wasio na wake; \v 30 nao wanaoomboleza, kama ambao hawaombolezi; wenye furaha kama wasiokuwa nayo; wale wanaonunua, kama vile vitu walivyonunua si mali yao; \v 31 nao wale wanaoshughulika na vitu vya dunia hii, kama ambao hawahusiki navyo. Kwa maana dunia hii kama tunavyoiona sasa inapita. \p \v 32 Ningetaka msiwe na masumbufu. Mwanaume ambaye hajaoa anajishughulisha na mambo ya Bwana Isa, jinsi ya kumpendeza Bwana Isa. \v 33 Lakini mwanaume aliyeoa anajishughulisha na mambo ya dunia, jinsi ya kumfurahisha mkewe, \v 34 na mawazo yake yamegawanyika. Mwanamke asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana: lengo lake ni awe mtakatifu kimwili na kiroho. Lakini yule aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia, jinsi atakavyoweza kumfurahisha mumewe. \v 35 Ninasema haya kwa faida yenu wenyewe, sio ili kuwawekea vizuizi bali mpate kuishi kwa jinsi ilivyo vyema bila kuvutwa pengine katika kujitoa kwenu kwa Bwana Isa. \p \v 36 Kama mtu yeyote anadhani kwamba hamtendei ilivyo sawa mwanamwali ambaye amemposa, naye akiwa umri wake unazidi kuendelea na mtu huyo anajisikia kwamba inampasa kuoa, afanye kama atakavyo. Yeye hatendi dhambi. Yawapasa waoane. \v 37 Lakini mwanaume ambaye ameamua moyoni mwake kutooa bila kulazimishwa na mtu yeyote, bali anaweza kuzitawala tamaa zake kutomwoa huyo mwanamwali, basi anafanya ipasavyo. \v 38 Hivyo basi, mwanaume amwoaye mwanamwali afanya vyema, lakini yeye asiyemwoa afanya vyema zaidi. \p \v 39 Mwanamke aliyeolewa amefungwa na sheria maadamu mumewe yu hai. Lakini mumewe akifa, basi mwanamke huyo yuko huru kuolewa na mume mwingine ampendaye, lakini lazima awe katika Bwana Isa. \v 40 Lakini kwa maoni yangu, angekuwa na furaha zaidi akibaki alivyo. Nami nadhani pia nina Roho wa Mungu. \c 8 \s1 Chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu \p \v 1 Sasa kuhusu chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu, tunajua kwamba “sisi sote tuna ujuzi.” Lakini ujuzi hujivuna, bali upendo hujenga. \v 2 Mtu yeyote anayedhani kwamba anajua kitu, bado hajui kama impasavyo kujua. \v 3 Lakini mtu ampendaye Mungu, hujulikana naye Mungu. \p \v 4 Hivyo basi, kuhusu kula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu: Tunajua kwamba “Sanamu si kitu chochote kabisa duniani,” na kwamba “Kuna Mungu mmoja tu.” \v 5 Kwa kuwa hata kama wapo hao wanaoitwa miungu, wakiwa mbinguni au duniani (kama ilivyo kweli wapo “miungu” wengi na “mabwana” wengi), \v 6 kwetu sisi yuko Mungu mmoja, aliye Baba\f + \fr 8:6 \fr*\ft Kwa mwanadamu, Mwenyezi Mungu ni Baba kupitia uhusiano unaopatikana katika kumtumaini Isa Al-Masihi.\ft*\f*, ambaye vitu vyote vyatoka kwake na kwa ajili yake sisi twaishi; na kuna Bwana mmoja tu, Isa Al-Masihi, ambaye kwa yeye vitu vyote vilitoka na kwa yeye tunaishi. \p \v 7 Lakini si wote wanaojua jambo hili. Baadhi ya watu bado wamezoea sanamu kuwa halisi hivi kwamba wanapokula chakula kama hicho wanadhani kimetolewa sadaka kwa sanamu na kwa kuwa dhamiri zao ni dhaifu, dhamiri yao inanajisika. \v 8 Lakini chakula hakituleti karibu na Mungu, wala hatupotezi chochote tusipokula, wala hatuongezi chochote tukila. \p \v 9 Lakini angalieni jinsi mnavyotumia uhuru wenu usije ukawa kikwazo kwao walio dhaifu. \v 10 Kwa maana kama mtu yeyote mwenye dhamiri dhaifu akiwaona ninyi wenye ujuzi huu mkila katika hekalu la sanamu, je, si atatiwa moyo kula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu? \v 11 Kwa njia hiyo, huyo ndugu mwenye dhamiri dhaifu, ambaye Al-Masihi alikufa kwa ajili yake, ataangamia kwa sababu ya ujuzi wenu. \v 12 Mnapotenda dhambi dhidi ya ndugu zenu kwa njia hii na kujeruhi dhamiri zao zilizo dhaifu, mnamkosea Al-Masihi. \v 13 Kwa hiyo, kama kile ninachokula kitamfanya ndugu yangu aanguke katika dhambi, sitakula nyama kamwe, nisije nikamfanya ndugu yangu aanguke. \c 9 \s1 Haki za Mtume Paulo \p \v 1 Je, mimi si huru? Je, mimi si mtume? Je, mimi sikumwona Isa, Bwana wetu? Je, ninyi si matunda ya kazi yangu katika Bwana? \v 2 Hata kama mimi si mtume kwa wengine, hakika mimi ni mtume kwenu, kwa maana ninyi ni muhuri wa utume wangu katika Bwana Isa. \p \v 3 Huu ndio utetezi wangu kwa hao wanaokaa kunihukumu. \v 4 Je, hatuna haki ya kula na kunywa? \v 5 Je, hatuna haki ya kusafiri na mke anayeamini, kama wanavyofanya mitume wengine na ndugu zake Bwana Isa na Kefa\f + \fr 9:5 \fr*\ft yaani \ft*\fqa Petro\fqa*\f*? \v 6 Au ni mimi na Barnaba tu inatubidi kufanya kazi ili tuweze kupata mahitaji yetu? \p \v 7 Ni askari yupi aendaye vitani kwa gharama zake mwenyewe? Ni nani apandaye shamba la mizabibu na asile matunda yake? Ni nani achungaye kundi na asipate maziwa yake. \v 8 Je, nasema mambo haya katika mtazamo wa kibinadamu tu? Je, Torati haisemi vivyo hivyo? \v 9 Kwa maana imeandikwa katika Torati ya Musa: “Usimfunge maksai kinywa apurapo nafaka.” Je, Mungu hapa anahusika na ng’ombe? \v 10 Je, Mungu hasemi haya hasa kwa ajili yetu? Hakika yameandikwa kwa ajili yetu, kwa sababu mtu anapolima na mpuraji akapura nafaka, wote wanapaswa kufanya hivyo wakiwa na tumaini la kushiriki mavuno. \v 11 Je, ikiwa sisi tulipanda mbegu ya kiroho miongoni mwenu, itakuwa ni jambo kubwa iwapo tutavuna vitu vya mwili kutoka kwenu? \v 12 Kama wengine wana haki ya kupata msaada kutoka kwenu, isingepasa tuwe na haki hiyo hata zaidi? \p Lakini sisi hatukutumia haki hii. Kinyume chake, tunavumilia kila kitu ili tusije tukazuia Injili ya Al-Masihi. \v 13 Je, hamjui kwamba, watu wafanyao kazi hekaluni hupata chakula chao kutoka hekaluni, nao wale wahudumiao madhabahuni hushiriki kile kitolewacho madhabahuni? \v 14 Vivyo hivyo, Bwana Isa ameamuru kwamba wale wanaohubiri Injili wapate riziki yao kutokana na Injili. \p \v 15 Lakini sijatumia hata mojawapo ya haki hizi. Nami siandiki haya nikitumaini kwamba mtanifanyia mambo hayo. Heri nife kuliko mtu yeyote kuninyima huku kujisifu kwangu. \v 16 Lakini ninapohubiri Injili siwezi kujisifu maana ninalazimika kuhubiri. Ole wangu nisipoihubiri Injili! \v 17 Nikihubiri kwa hiari, ninayo thawabu. Lakini kama si kwa hiari, basi ninachofanya ni kutekeleza tu uwakili niliowekewa. \v 18 Basi je, thawabu yangu ni nini? Thawabu yangu ni hii: Ya kwamba katika kuhubiri Injili niitoe bila gharama, bila kutumia kwa utimilifu uwezo wangu nilio nao katika Injili. \p \v 19 Ingawa mimi ni huru, wala si mtumwa wa mtu yeyote, nimejifanya mtumwa wa kila mtu, ili niweze kuwavuta wengi kadiri iwezekanavyo. \v 20 Kwa Wayahudi, nilikuwa kama Myahudi, ili niwapate Wayahudi. Kwa watu wale walio chini ya Torati, nilikuwa kama aliye chini ya Torati (ingawa mimi siko chini ya Torati), ili niweze kuwapata wale walio chini ya Torati. \v 21 Kwa watu wasio na Torati nilikuwa kama asiye na Torati (ingawa siko huru mbali na Torati ya Mungu, bali niko chini ya sheria ya Al-Masihi), ili niweze kuwapata wale wasio na sheria. \v 22 Kwa walio dhaifu nilikuwa dhaifu, ili niweze kuwapata walio dhaifu. Nimekuwa mtu wa hali zote kwa watu wote ili kwa njia yoyote niweze kuwaokoa baadhi yao. \v 23 Nafanya haya yote kwa ajili ya Injili, ili nipate kushiriki baraka zake. \p \v 24 Je, hamjui kwamba katika mashindano ya mbio wote wanaoshindana hukimbia, lakini ni mmoja wao tu apewaye tuzo? Kwa hiyo kimbieni katika mashindano ili mkapata tuzo. \p \v 25 Kila mmoja anayeshiriki katika mashindano hufanya mazoezi makali. Wao hufanya hivyo ili wapokee taji lisilodumu, lakini sisi tunafanya hivyo ili kupata taji linalodumu milele. \v 26 Kwa hiyo mimi sikimbii kama mtu akimbiaye bila lengo, sipigani kama mtu anayepiga hewa. \v 27 La, bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha, ili nikiisha kuwahubiria wengine, nisije nikakataliwa. \c 10 \s1 Onyo kutoka historia ya Waisraeli \p \v 1 Ndugu zangu, sitaki mkose kufahamu ukweli huu kwamba baba zetu walikuwa wote chini ya wingu na kwamba wote walipita katikati ya bahari. \v 2 Wote wakabatizwa kuwa wa Musa ndani ya lile wingu na ndani ya ile bahari. \v 3 Wote walikula chakula kile kile cha roho, \v 4 na wote wakanywa kile kile kinywaji cha roho, kwa maana walikunywa kutoka ule mwamba wa roho uliofuatana nao, nao ule mwamba ulikuwa Al-Masihi. \v 5 Lakini Mungu hakupendezwa na wengi wao, kwa hiyo miili yao ilitapakaa jangwani. \p \v 6 Basi mambo haya yalifanyika kama mifano ili kutuzuia tusiweke mioyo yetu katika mambo maovu kama wao walivyofanya. \v 7 Msiwe waabudu sanamu, kama baadhi yao walivyokuwa, kama ilivyoandikwa, “Watu waliketi chini kula na kunywa, kisha wakainuka kucheza na kufanya sherehe za kipagani.” \v 8 Wala tusifanye uzinzi kama baadhi yao walivyofanya, wakafa watu elfu ishirini na tatu kwa siku moja. \v 9 Wala tusimjaribu Al-Masihi, kama baadhi yao walivyofanya, wakafa kwa kuumwa na nyoka. \v 10 Msinung’unike kama baadhi yao walivyofanya, wakaangamizwa na malaika mharibifu. \p \v 11 Mambo haya yote yaliwapata wao ili yawe mifano kwa wengine, nayo yaliandikwa ili yatuonye sisi ambao mwisho wa nyakati umetufikia. \v 12 Hivyo, yeye ajidhaniaye amesimama, aangalie asianguke. \v 13 Hakuna jaribu lolote lililowapata ambalo si la kawaida kwa wanadamu. Naye Mungu ni mwaminifu; hataruhusu mjaribiwe kupita mnavyoweza. Lakini mnapojaribiwa atawapa njia ya kushinda ili mweze kustahimili. \s1 Karamu za sanamu na Chakula cha Bwana Isa \p \v 14 Kwa hiyo wapendwa wangu, zikimbieni ibada za sanamu. \v 15 Nasema watu wenye ufahamu, amueni wenyewe kuhusu haya niyasemayo. \v 16 Je, kikombe cha baraka ambacho tunakibariki, si ushirika katika damu ya Al-Masihi? Mkate tunaoumega, si ushirika wa mwili wa Al-Masihi? \v 17 Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja, kwa kuwa wote twashiriki mkate mmoja. \p \v 18 Waangalieni watu wa Israeli: Je, wale wote walao dhabihu si ni wale watendao kazi madhabahuni? \v 19 Je, nina maana kwamba sadaka iliyotolewa kwa sanamu ni kitu chenye maana yoyote? Au kwamba sanamu ni kitu chenye maana yoyote? \v 20 La hasha! Lakini sadaka za watu wasiomjua Mungu hutolewa kwa mashetani, wala si kwa Mungu. Nami sitaki ninyi mwe na ushirika na mashetani. \v 21 Hamwezi kunywa katika kikombe cha Bwana Isa na cha mashetani pia. Hamwezi kuwa na sehemu katika Chakula cha Bwana Isa na katika chakula cha mashetani pia. \v 22 Je, tunataka kuamsha wivu wa Mwenyezi Mungu? Je, sisi tuna nguvu kuliko yeye? \s1 Fanyeni yote kwa utukufu wa Mwenyezi Mungu \p \v 23 “Vitu vyote ni halali,” lakini si vitu vyote vilivyo na faida. “Vitu vyote ni halali,” lakini si vyote vinavyojenga. \v 24 Mtu yeyote asitafute yaliyo yake mwenyewe, bali kila mtu atafute yale yanayowafaa wengine. \p \v 25 Kuleni chochote kinachouzwa sokoni, bila kuuliza swali lolote kwa ajili ya dhamiri. \v 26 Kwa maana, “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Mwenyezi Mungu.” \p \v 27 Ukikaribishwa chakula na mtu asiyeamini nawe ukikubali kwenda, kula kila kitu kitakachowekwa mbele yako bila kuuliza maswali kwa ajili ya dhamiri. \v 28 Lakini kama mtu yeyote akikuambia, “Hiki kimetolewa sadaka kwa sanamu,” basi usikile kwa ajili ya huyo aliyekuambia na kwa ajili ya dhamiri. \v 29 Nina maana dhamiri ya huyo aliyekuambia, wala si kwa ajili ya dhamiri yako. Lakini kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine? \v 30 Nikila kwa shukrani, kwa nini nashutumiwa kwa ajili ya kile ambacho ninamshukuria Mungu? \p \v 31 Basi, lolote mfanyalo, kama ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu. \v 32 Msiwe kikwazo kwa mtu yeyote, wawe Wayahudi au Wayunani, au kwa kundi la waumini la Mungu, \v 33 kama hata mimi ninavyojaribu kumpendeza kila mtu kwa kila namna. Kwa maana sitafuti mema kwa ajili yangu mwenyewe bali kwa ajili ya wengi, ili waweze kuokolewa. \c 11 \p \v 1 Igeni mfano wangu, kama ninavyouiga mfano wa Al-Masihi. \s1 Utaratibu katika ibada \p \v 2 Ninawasifu kwa kunikumbuka katika kila jambo na kwa kushika mapokeo kama nilivyowapatia. \p \v 3 Napenda mfahamu kwamba kichwa cha kila mwanaume ni Al-Masihi, na kichwa cha mwanamke ni mwanaume, nacho kichwa cha Al-Masihi ni Mungu. \v 4 Kila mwanaume anayeomba au kutoa unabii akiwa amefunika kichwa chake, anakiaibisha kichwa chake. \v 5 Naye kila mwanamke anayeomba au kutoa unabii pasipo kufunika kichwa chake, anakiaibisha kichwa chake, kwani ni sawa na yeye aliyenyoa nywele. \v 6 Kama mwanamke hatajifunika kichwa chake, basi inampasa kunyoa nywele zake. Lakini kama ni aibu kwa mwanamke kukata au kunyoa nywele zake, basi afunike kichwa chake. \p \v 7 Haimpasi mwanaume kufunika kichwa chake kwa kuwa yeye ni mfano wa Mungu na utukufu wa Mungu; lakini mwanamke ni utukufu wa mwanaume. \v 8 Kwa maana mwanaume hakutoka kwa mwanamke, bali mwanamke alitoka kwa mwanaume. \v 9 Wala mwanaume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke kwa ajili ya mwanaume. \v 10 Kwa sababu hii na kwa sababu ya malaika, inampasa mwanamke awe na ishara ya mamlaka juu yake. \v 11 Lakini katika Bwana Isa, mwanamke hajitegemei pasipo mwanaume na mwanaume hajitegemei pasipo mwanamke. \v 12 Kama vile mwanamke alivyoumbwa kutoka kwa mwanaume, vivyo hivyo mwanaume huzaliwa na mwanamke. Lakini vitu vyote vyatoka kwa Mungu. \p \v 13 Hukumuni ninyi wenyewe: Je, inafaa kwa mwanamke kumwomba Mungu bila kufunika kichwa chake? \v 14 Je, maumbile ya asili hayatufundishi kuwa ni aibu kwa mwanaume kuwa na nywele ndefu? \v 15 Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni utukufu kwake? Kwa maana mwanamke amepewa nywele ndefu ili kumfunika. \v 16 Kama mtu anataka kubishana kuhusu jambo hili, sisi wala makundi ya waumini ya Mungu hatutambui desturi nyingine. \s1 Matumizi mabaya ya Chakula cha Bwana Isa \p \v 17 Basi katika maagizo yafuatayo, siwezi kuwasifu, kwa sababu mkutanikapo si kwa ajili ya faida bali kwa hasara. \v 18 Kwanza, mnapokutana kama kundi la waumini, nasikia kwamba kuna mgawanyiko miongoni mwenu, nami kwa kiasi fulani nasadiki kuwa ndivyo ilivyo. \v 19 Bila shaka lazima pawe na tofauti miongoni mwenu ili kuonesha ni nani anayekubaliwa na Mungu. \v 20 Mkutanikapo pamoja si Chakula cha Bwana Isa mnachokula, \v 21 kwa kuwa mnapokula, kila mmoja wenu anakula bila kuwangoja wengine. Mmoja hukaa njaa na mwingine analewa. \v 22 Je, hamna nyumbani kwenu ambako mnaweza kula na kunywa? Au mnalidharau kundi la waumini la Mungu na kuwadhalilisha wale wasio na kitu? Niwaambie nini? Je, niwasifu kuhusu jambo hili? La, hasha! \s1 Kushiriki Chakula cha Bwana Isa \r (Mathayo 26:26-29; Marko 14:22-25; Luka 22:14-20) \p \v 23 Kwa maana mimi nilipokea kutoka kwa Bwana Isa yale niliyowapa ninyi, kwamba Bwana Isa, usiku ule aliposalitiwa, alitwaa mkate, \v 24 naye baada ya kushukuru, akaumega, akasema, “Huu ndio mwili wangu, uliotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.” \v 25 Vivyo hivyo baada ya kula, akakitwaa kikombe, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu. Fanyeni hivi kila mnywapo, kwa ukumbusho wangu.” \v 26 Maana kila mlapo mkate huu na kunywea kikombe hiki, mnatangaza mauti ya Bwana Isa hadi ajapo. \s1 Kushiriki Chakula cha Bwana Isa isivyostahili \p \v 27 Kwa hiyo, mtu yeyote alaye mkate huo au kukinywea kikombe hicho cha Bwana Isa isivyostahili, atakuwa na hatia ya dhambi juu ya mwili na damu ya Bwana Isa. \v 28 Inampasa mtu ajichunguze mwenyewe, kabla ya kula mkate na kukinywea kikombe. \v 29 Kwa maana mtu yeyote alaye na kunywa pasipo kuutambua mwili wa Bwana Isa, hula na kunywa hukumu juu yake mwenyewe. \v 30 Hii ndiyo sababu wengi miongoni mwenu ni wagonjwa na dhaifu na wengine wenu hata wamekufa. \v 31 Lakini kama tungejichunguza wenyewe tusingehukumiwa. \v 32 Tunapohukumiwa na Bwana Isa, tunaadibishwa ili tusije tukahukumiwa pamoja na ulimwengu. \p \v 33 Kwa hiyo, ndugu zangu, mkutanikapo pamoja ili kula, mngojane. \v 34 Kama mtu akiwa na njaa, ale nyumbani mwake ili mkutanapo pamoja msije mkahukumiwa. \p Nami nitakapokuja nitawapa maelekezo zaidi. \c 12 \s1 Karama za rohoni \p \v 1 Basi ndugu zangu, kuhusu karama za rohoni, sitaki mkose kufahamu. \v 2 Mnajua kwamba mlipokuwa watu wasiomjua Mungu, kwa njia moja au nyingine mlishawishika na kupotoshwa mkielekezwa kwa sanamu zisizonena. \v 3 Kwa hiyo nawaambieni ya kuwa hakuna mtu anayeongozwa na Roho Mtakatifu wa Mungu anayeweza kusema, “Isa na alaaniwe.” Pia hakuna mtu awezaye kusema, “Isa ni Bwana,” isipokuwa ameongozwa na Roho wa Mungu. \p \v 4 Kuna aina mbalimbali za karama, lakini Roho ni yule yule. \v 5 Kuna huduma za aina mbalimbali, lakini Bwana Isa ni yule yule. \v 6 Kisha kuna tofauti za kutenda kazi, lakini ni Mungu yule yule atendaye kazi zote kwa watu wote. \p \v 7 Basi kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho wa Mungu kwa faida ya wote. \v 8 Maana mtu mmoja kwa Roho hupewa neno la hekima na mwingine neno la maarifa kwa Roho huyo huyo. \v 9 Mtu mwingine imani kwa huyo Roho na mwingine karama za kuponya kwa huyo Roho mmoja. \v 10 Kwa mwingine matendo ya miujiza, kwa mwingine unabii, kwa mwingine kupambanua roho, kwa mwingine kunena aina mbalimbali za lugha, na kwa mwingine bado, tafsiri za lugha. \v 11 Haya yote hufanywa na huyo huyo Roho mmoja, Roho naye humgawia kila mtu, kama apendavyo. \s1 Mwili mmoja wenye viungo vingi \p \v 12 Kama vile mwili ulivyo mmoja nao una viungo vingi; navyo viungo vyote vya mwili ingawa ni vingi, ni mwili mmoja; vivyo hivyo na Al-Masihi. \v 13 Kwa maana katika Roho mmoja wa Mungu wote tulibatizwa katika mwili mmoja, kama ni Wayahudi au Wayunani, kama ni watumwa au watu huru, nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja. \p \v 14 Basi mwili si kiungo kimoja, bali ni viungo vingi. \v 15 Kama mguu ungesema, “Kwa kuwa mimi si mkono basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya huo mguu usiwe sehemu ya mwili. \v 16 Na kama sikio lingesema, “Kwa kuwa mimi si jicho, basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya hilo sikio lisiwe sehemu ya mwili. \v 17 Kama mwili wote ungakuwa jicho tu, kusikia kungekuwa wapi? Au kama mwili wote ungekuwa sikio, kunusa kungekuwa wapi? \v 18 Lakini kama ilivyo, Mungu ameweka viungo katika mwili, kila kimoja kama alivyopenda. \v 19 Kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi? \v 20 Kama ulivyo, una viungo vingi, lakini mwili ni mmoja. \p \v 21 Jicho haliwezi kuuambia mkono, “Sina haja nawe!” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, “Sina haja na ninyi!” \v 22 Lakini badala yake, vile viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu, ndivyo ambavyo ni vya muhimu sana. \v 23 Navyo vile viungo tunavyoviona havina heshima, ndivyo tunavipa heshima maalum. Vile viungo vya mwili ambavyo havina uzuri, tunavipa heshima ya pekee; \v 24 wakati vile viungo vyenye uzuri havihitaji utunzaji wa pekee. Lakini Mungu ameviweka pamoja viungo vya mwili na akavipa heshima zaidi vile vilivyopungukiwa, \v 25 ili pasiwe na mafarakano katika mwili, bali viungo vyote vihudumiane kwa usawa kila kimoja na mwenzake. \v 26 Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia pamoja nacho; kama kiungo kimoja kikipewa heshima, viungo vyote hufurahi pamoja nacho. \p \v 27 Sasa ninyi ni mwili wa Al-Masihi na kila mmoja wenu ni sehemu ya huo mwili. \v 28 Mungu ameweka katika jumuiya ya waumini kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu, kisha watenda miujiza, pia karama za kuponya, karama za kusaidiana, karama za uongozi, na aina mbalimbali za lugha. \v 29 Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote wanatenda miujiza? \v 30 Je, wote wana karama ya kuponya? Je, wote hunena kwa lugha mpya? Je, wote wanatafsiri? \v 31 Basi tamanini sana karama zilizo kuu. \p Nami nitawaonesha njia iliyo bora zaidi. \c 13 \s1 Karama ya upendo \p \v 1 Hata kama nikisema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa kengele inayolia au toazi linalovuma. \v 2 Ningekuwa na karama ya unabii na kujua siri zote na maarifa yote, hata kama nina imani kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, mimi si kitu. \v 3 Nikitoa mali yote niliyo nayo, na nikijitolea mwili wangu uchomwe moto, kama sina upendo, hainifaidi kitu. \p \v 4 Upendo huvumilia, upendo hufadhili, upendo hauoni wivu, hauna majivuno, hauna kiburi. \v 5 Haukosi kuwa na adabu, hautafuti mambo yake, haukasiriki upesi, hauweki kumbukumbu ya mabaya. \v 6 Upendo haufurahii mabaya bali hufurahi pamoja na kweli. \v 7 Upendo huvumilia yote, huamini yote, hutumaini yote, hustahimili yote. \p \v 8 Upendo haushindwi kamwe. Lakini ukiwepo unabii, utakoma; zikiwepo lugha, zitakoma; yakiwepo maarifa, yatapita. \v 9 Kwa maana tunafahamu kwa sehemu na tunatoa unabii kwa sehemu. \v 10 Lakini ukamilifu ukija, yale yasiyo kamili hutoweka. \v 11 Nilipokuwa mtoto, nilisema kama mtoto, niliwaza kama mtoto, nilifikiri kama mtoto. Nilipokuwa mtu mzima niliacha mambo ya kitoto. \v 12 Kwa maana sasa tunaona taswira kama kwa kioo, lakini wakati huo tutaona wazi. Sasa nafahamu kwa sehemu, wakati huo nitafahamu kikamilifu, kama vile mimi ninavyofahamika kikamilifu. \p \v 13 Basi sasa, yanadumu mambo haya matatu: Imani, tumaini na upendo. Lakini lililo kuu miongoni mwa haya matatu ni upendo. \c 14 \s1 Karama za unabii na lugha \p \v 1 Fuateni upendo na kutaka sana karama za roho, hasa karama ya unabii. \v 2 Kwa maana mtu yeyote anayesema kwa lugha, hasemi na wanadamu bali anasema na Mungu. Kwa kuwa hakuna mtu yeyote anayemwelewa, kwani anasema mambo ya siri kwa roho. \v 3 Lakini anayetoa unabii anasema na watu akiwajenga, kuwatia moyo na kuwafariji. \v 4 Anenaye kwa lugha hujijenga mwenyewe, bali atoaye unabii huwajenga waumini. \v 5 Ningependa kila mmoja wenu anene kwa lugha, lakini ningependa zaidi nyote mtoe unabii. Kwa kuwa yeye atoaye unabii ni mkuu kuliko anenaye kwa lugha, isipokuwa atafsiri, ili waumini wote wapate kujengwa. \p \v 6 Sasa ndugu zangu, nikija kwenu nikasema kwa lugha mpya, nitawafaidia nini kama sikuwaletea ufunuo au neno la maarifa au unabii au mafundisho? \v 7 Hata vitu visivyo na uhai vitoapo sauti, kama vile filimbi au kinubi, mtu atajuaje ni wimbo gani unaoimbwa kusipokuwa na tofauti ya upigaji? \v 8 Tena kama tarumbeta haitoi sauti inayoeleweka, ni nani atakayejiandaa kwa ajili ya vita? \v 9 Vivyo hivyo na ninyi, mkinena maneno yasiyoeleweka katika akili, mtu atajuaje mnalosema? Kwa maana mtakuwa mnasema hewani tu. \v 10 Bila shaka ziko sauti nyingi ulimwenguni, wala hakuna isiyo na maana. \v 11 Basi kama sielewi maana ya hiyo sauti, nitakuwa mgeni kwa yule msemaji, naye atakuwa mgeni kwangu. \v 12 Vivyo hivyo na ninyi. Kwa kuwa mnatamani kuwa na karama za rohoni, jitahidini kuzidi sana katika karama kwa ajili ya kuwajenga waumini. \p \v 13 Kwa sababu hii, yeye anenaye kwa lugha na aombe kwamba apate kutafsiri kile anachonena. \v 14 Kwa maana nikiomba kwa lugha, roho yangu inaomba, lakini akili yangu haina matunda. \v 15 Nifanyeje basi? Nitaomba kwa roho, na pia nitaomba kwa akili yangu. Nitaimba kwa roho na nitaimba kwa akili yangu pia. \v 16 Ikiwa unabariki kwa roho, mtu mwingine atakayejikuta miongoni mwa hao wasiojua, atawezaje kusema “Amen” katika kushukuru kwako, wakati haelewi unachosema? \v 17 Mnaweza kuwa mnatoa shukrani kweli, sawa, lakini huyo mtu mwingine hajengeki. \p \v 18 Namshukuru Mungu kwamba mimi nanena kwa lugha kuliko ninyi nyote. \v 19 Lakini katika kundi la waumini ni afadhali niseme maneno matano ya kueleweka ili niwafundishe wengine kuliko kusema maneno elfu kumi kwa lugha. \p \v 20 Ndugu zangu, msiwe kama watoto katika kufikiri kwenu, afadhali kuhusu uovu mwe kama watoto wachanga, lakini katika kufikiri kwenu, mwe watu wazima. \v 21 Katika Torati imeandikwa kwamba: \q1 “Kupitia kwa watu wenye lugha ng’eni \q2 na kupitia midomo ya wageni, \q1 nitasema na watu hawa, \q2 lakini hata hivyo hawatanisikiliza, \q2 asema Mwenyezi Mungu.” \p \v 22 Basi kunena kwa lugha ni ishara, si kwa waaminio, bali kwa wasioamini, wakati unabii si kwa ajili ya wasioamini, bali kwa ajili ya waaminio. \v 23 Kwa hiyo kama kundi la waumini wote wakikutana na kila mmoja akanena kwa lugha, kisha wakaingia wageni wasioelewa au wasioamini, je, hawatasema kwamba wote mna wazimu? \v 24 Lakini kama mtu asiyeamini au asiyeelewa akiingia wakati kila mtu anatoa unabii, ataaminishwa na watu wote kuwa yeye ni mwenye dhambi na kuhukumiwa na wote, \v 25 nazo siri za moyo wake zitawekwa wazi. Kwa hiyo ataanguka chini na kumwabudu Mungu akikiri, “Kweli Mungu yuko kati yenu!” \s1 Kumwabudu Mwenyezi Mungu kwa utaratibu \p \v 26 Basi tuseme nini ndugu zangu? Mnapokutana pamoja, kila mmoja ana wimbo, au neno la mafundisho, au ufunuo, lugha mpya au atatafsiri. Mambo yote yatendeke kwa ajili ya kulijenga kundi la waumini. \v 27 Kama mtu yeyote akinena kwa lugha, basi waseme watu wawili au watatu, si zaidi, mmoja baada ya mwingine, na lazima awepo mtu wa kutafsiri. \v 28 Lakini kama hakuna mtu wa kutafsiri, hao watu na wanyamaze kimya katika kundi la waumini, na wanene na nafsi zao wenyewe na Mungu. \p \v 29 Manabii wawili au watatu wanene, na wengine wapime kwa makini yale yasemwayo. \v 30 Kama mtu yeyote aliyeketi karibu, akipata ufunuo, basi yule wa kwanza na anyamaze. \v 31 Kwa maana wote mnaweza kutoa unabii, mmoja baada ya mwingine, ili kila mtu apate kufundishwa na kutiwa moyo. \v 32 Roho za manabii huwatii manabii. \v 33 Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko bali ni Mungu wa amani. \p Kama ilivyo katika makusanyiko yote ya watakatifu, \v 34 wanawake wanapaswa kuwa kimya katika kundi la waumini. Hawaruhusiwi kusema, bali wanyenyekee kama Torati isemavyo. \v 35 Wakitaka kuuliza kuhusu jambo lolote, wawaulize waume zao nyumbani. Kwa maana ni aibu kwa mwanamke kuzungumza katika kundi la waumini. \p \v 36 Je, neno la Mungu lilianzia kwenu? Au ni ninyi tu ambao neno la Mungu limewafikia? \v 37 Kama mtu yeyote akidhani kwamba yeye ni nabii, au ana karama za rohoni, basi na akubali kwamba haya ninayoandika ni maagizo kutoka kwa Bwana Isa. \v 38 Kama mtu akipuuza jambo hili yeye mwenyewe atapuuzwa. \p \v 39 Kwa hiyo ndugu zangu, takeni sana kutoa unabii na msikataze watu kusema kwa lugha. \v 40 Lakini kila kitu kitendeke kwa ufasaha na kwa utaratibu. \c 15 \s1 Kufufuka kwa Al-Masihi \p \v 1 Basi ndugu zangu nataka niwakumbushe kuhusu Injili niliyowahubiria, mkaipokea na ambayo katika hiyo mmesimama. \v 2 Kwa Injili hii mnaokolewa mkishikilia kwa uthabiti neno nililowahubiria ninyi. La sivyo, mmeamini katika ubatili. \p \v 3 Kwa maana yale niliyopokea ndiyo niliyowapa ninyi, kama yenye umuhimu wa kwanza: Kwamba Al-Masihi alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama Maandiko yanavyosema, \v 4 ya kuwa alizikwa na alifufuliwa siku ya tatu, kama Maandiko yanavyosema, \v 5 na kwamba alimtokea Kefa\f + \fr 15:5 \fr*\ft yaani \ft*\fqa Petro\fqa*\f*, kisha akawatokea wale kumi na wawili. \v 6 Baadaye akawatokea wale ndugu waumini zaidi ya mia tano kwa pamoja, ambao wengi wao bado wako hai, ingawa wengine wamelala. \v 7 Ndipo akamtokea Yakobo na kisha mitume wote. \v 8 Mwisho wa wote, akanitokea mimi pia, ambaye ni kama aliyezaliwa si kwa wakati wake. \p \v 9 Kwa maana mimi ndiye mdogo kuliko mitume wote, nisiyestahili kuitwa mtume, kwa sababu niliwatesa waumini wa Mungu. \v 10 Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo, na neema yake kwangu haikuwa kitu bure. Bali nilizidi sana kufanya kazi kuliko mitume wote, lakini haikuwa mimi, bali ni ile neema ya Mungu iliyokuwa pamoja nami. \v 11 Hivyo basi, kama ilikuwa mimi au wao, hili ndilo tunalohubiri, na hili ndilo mliloamini. \s1 Ufufuo wa wafu \p \v 12 Basi kama tumehubiri kwamba Al-Masihi alifufuliwa kutoka kwa wafu, mbona baadhi yenu mnasema hakuna ufufuo wa wafu? \v 13 Lakini kama hakuna ufufuo wa wafu, basi hata Al-Masihi hakufufuliwa. \v 14 Tena ikiwa Al-Masihi hakufufuliwa kutoka kwa wafu, kuhubiri kwetu kumekuwa ni bure na imani yenu ni batili. \v 15 Zaidi ya hayo, twaonekana kuwa mashahidi wa uongo kuhusu Mungu, kwa sababu tumeshuhudia kumhusu Mungu kwamba alimfufua Al-Masihi kutoka kwa wafu, lakini hilo haliwezi kuwa kweli kama wafu hawafufuliwi. \v 16 Kwa kuwa kama wafu hawafufuliwi, basi hata Al-Masihi hajafufuka. \v 17 Tena kama Al-Masihi hajafufuliwa, imani yenu ni batili; nanyi bado mko katika dhambi zenu. \v 18 Hivyo basi, wote waliolala katika Al-Masihi wamepotea. \v 19 Ikiwa tumaini letu ndani ya Al-Masihi ni kwa ajili ya maisha haya tu, sisi tunastahili kuhurumiwa kuliko watu wote. \p \v 20 Lakini kweli Al-Masihi amefufuliwa kutoka kwa wafu, tunda la kwanza la wale wote waliolala. \v 21 Kwa maana kama vile mauti ilivyokuja kupitia kwa mtu mmoja, vivyo hivyo, ufufuo wa wafu umekuja kupitia kwa mtu mmoja. \v 22 Kwa maana kama vile katika Adamu watu wote wanakufa, vivyo hivyo katika Al-Masihi wote watafanywa hai. \v 23 Lakini kila mmoja kwa wakati wake: Al-Masihi, tunda la kwanza kisha, wale walio wake, wakati atakapokuja. \v 24 Ndipo mwisho utafika, atakapomkabidhi Mungu Baba\f + \fr 15:24 \fr*\ft Jina Baba linaonesha uhusiano maalum wa Isa na Mwenyezi Mungu. Kwa mwanadamu, Mwenyezi Mungu ni Baba kupitia uhusiano unaopatikana katika kumtumaini Isa Al-Masihi.\ft*\f* Mwenyezi ufalme, baada ya kuangamiza kila utawala na kila mamlaka na nguvu. \v 25 Kwa maana lazima Al-Masihi atawale hadi awe amewaweka adui zake wote chini ya miguu yake. \v 26 Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni mauti. \v 27 Kwa maana Mungu “ameweka vitu vyote chini ya miguu yake”. Lakini isemapo kwamba “vitu vyote” vimewekwa chini yake, ni wazi kwamba Mungu aliyetiisha vitu vyote chini ya Al-Masihi hayumo miongoni mwa hivyo vilivyotiishwa. \v 28 Atakapokuwa amekwisha kuyafanya haya, ndipo Mwana mwenyewe atatiishwa chini yake yeye aliyetiisha vitu vyote, ili Mungu awe yote katika yote. \p \v 29 Basi kama hakuna ufufuo, watafanyaje wale wabatizwao kwa ajili ya wafu? Kama wafu hawafufuliwi kamwe, mbona watu wanabatizwa kwa ajili yao? \v 30 Nasi kwa upande wetu kwa nini tunajihatarisha kila saa? \v 31 Kama majivuno yangu kwa ajili yenu katika Al-Masihi Isa Bwana wetu ni kweli, ndugu zangu, ninakufa kila siku. \v 32 Kama kwa sababu za kibinadamu tu nilipigana na wanyama wakali huko Efeso, ningekuwa nimepata faida gani? Kama wafu hawafufuliwi, \q1 “Tuleni na kunywa, \q2 kwa kuwa kesho tutakufa.” \m \v 33 Msidanganyike: “Ushirika na watu wabaya huharibu tabia njema.” \v 34 Zindukeni mwe na akili kama iwapasavyo, wala msitende dhambi tena; kwa maana watu wengine hawamjui Mungu. Nasema mambo haya ili mwone aibu. \s1 Mwili wa ufufuo \p \v 35 Lakini mtu anaweza kuuliza, “Wafu wafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani?” \v 36 Ninyi wapumbavu kiasi gani? Mpandacho hakiwi hai kama hakikufa. \v 37 Mpandapo, hampandi mwili ule utakao kuwa, bali mwapanda mbegu tu, pengine ya ngano au ya kitu kingine. \v 38 Lakini Mungu huipa mbegu umbo kama alivyokusudia mwenyewe na kila aina ya mbegu huipa umbo lake. \v 39 Kwa maana nyama zote si za aina moja. Binadamu wana nyama ya aina moja, wanyama wana aina nyingine, kadhalika ndege na samaki wana nyama tofauti. \v 40 Pia kuna miili ya mbinguni na miili ya duniani, lakini fahari ya ile miili ya mbinguni ni ya aina moja, na fahari ya ile miili ya duniani ni ya aina nyingine. \v 41 Jua lina fahari ya aina moja, mwezi nao una fahari yake na nyota pia, nazo nyota hutofautiana katika fahari. \p \v 42 Hivyo ndivyo itakavyokuwa wakati wa ufufuo wa wafu. Ule mwili wa kuharibika uliopandwa, utafufuliwa usioharibika; \v 43 unapandwa katika aibu, unafufuliwa katika utukufu, unapandwa katika udhaifu, unafufuliwa katika nguvu, \v 44 unapandwa mwili wa asili, unafufuliwa mwili wa kiroho. \p Kama kuna mwili wa asili, basi kuna mwili wa kiroho pia. \v 45 Kwa hiyo imeandikwa, “Mtu wa kwanza Adamu alifanyika kiumbe hai”; Adamu wa mwisho, yeye ni roho iletayo uzima. \v 46 Lakini si ule wa kiroho uliotangulia, bali ni ule wa asili, kisha ule wa kiroho. \v 47 Mtu wa kwanza aliumbwa kwa mavumbi ya ardhini, mtu wa pili alitoka mbinguni. \v 48 Kama vile alivyokuwa yule wa ardhini, ndivyo walivyo wale walio wa ardhini; na kwa vile alivyo mtu yule aliyetoka mbinguni, ndivyo walivyo wale walio wa mbinguni. \v 49 Kama vile tulivyochukua mfano wa mtu wa ardhini, ndivyo tutakavyochukua mfano wa yule mtu aliyetoka mbinguni. \p \v 50 Ndugu zangu nisemalo ni hili: mwili na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu, wala kuharibika kurithi kutokuharibika. \v 51 Sikilizeni, nawaambia siri: Sote hatutalala, lakini sote tutabadilishwa: \v 52 ghafula, kufumba na kufumbua, parapanda ya mwisho itakapolia. Kwa kuwa parapanda italia, nao wafu watafufuliwa na miili isiyoharibika, nasi tutabadilishwa. \v 53 Kwa maana mwili huu wa kuharibika lazima uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa lazima uvae kutokufa. \v 54 Kwa hiyo, mwili huu wa kuharibika utakapovaa kutokuharibika, nao huu mwili wa kufa utakapovaa kutokufa, ndipo lile neno lililoandikwa litakapotimia: “Mauti imemezwa kwa kushinda.” \q1 \v 55 “Kuko wapi, ee mauti, kushinda kwako? \q2 Uko wapi, ee mauti, uchungu wako?” \m \v 56 Uchungu wa mauti ni dhambi na nguvu ya dhambi ni sheria. \v 57 Lakini Mungu apewe shukrani, yeye atupaye ushindi kupitia kwa Bwana wetu Isa Al-Masihi. \p \v 58 Kwa hiyo, ndugu zangu wapendwa, simameni imara. Msitikisike. Mzidi sana katika kuitenda kazi ya Bwana Isa, kwa maana mnajua ya kuwa, kazi yenu katika Bwana Isa si bure. \c 16 \s1 Changizo kwa ajili ya watakatifu \p \v 1 Basi kuhusu changizo kwa ajili ya watakatifu: Kama nilivyoyaagiza makundi ya waumini ya Galatia, fanyeni vivyo hivyo. \v 2 Siku ya kwanza ya kila juma, kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha, kulingana na mapato yake, na fedha hizo aziweke akiba, ili nitakapokuja pasiwe na lazima ya kufanya mchango. \v 3 Kwa hiyo nitakapowasili, nitawapa wale mtakaowachagua barua za kuwatambulisha, ili kuwatuma wapeleke zawadi zenu huko Yerusalemu. \v 4 Ikionekana ni vyema na mimi niende, basi hao watu watafuatana nami. \s1 Mahitaji binafsi \p \v 5 Baada ya kupitia Makedonia nitakuja kwenu, maana ninakusudia kupitia Makedonia. \v 6 Huenda nitakaa nanyi kwa muda, au hata kukaa nanyi kipindi chote cha baridi, ili mweze kunisaidia katika safari yangu, popote niendapo. \v 7 Kwa maana sitaki niwaone sasa na kupita tu; natarajia kuwa nanyi kwa muda wa kutosha, kama Bwana Isa akipenda. \v 8 Lakini nitakaa Efeso hadi wakati wa Pentekoste, \v 9 kwa maana mlango mkubwa umefunguliwa kwangu kufanya kazi yenye matunda, nako huko kuna adui wengi wanaonipinga. \p \v 10 Ikiwa Timotheo atakuja kwenu, hakikisheni kwamba hana hofu yoyote akiwa nanyi, kwa sababu anafanya kazi ya Bwana Isa, kama mimi nifanyavyo. \v 11 Basi asiwepo mtu atakayekataa kumpokea. Msafirisheni kwa amani ili aweze kunijia tena. Namtarajia pamoja na ndugu. \p \v 12 Basi kwa habari za ndugu yetu Apolo, nimemsihi kwa bidii aje kwenu pamoja na hao ndugu. Ingawa alikuwa hapendi kabisa kuja sasa, lakini atakuja apatapo nafasi. \s1 Maneno ya mwisho \p \v 13 Kesheni; simameni imara katika imani; kuweni mashujaa na hodari. \v 14 Fanyeni kila kitu katika upendo. \p \v 15 Ninyi mnajua kwamba watu wa nyumbani mwa Stefana ndio walikuwa wa kwanza kuamini katika Akaya, nao wamejitoa kwa ajili ya kuwahudumia watakatifu. Ndugu nawasihi, \v 16 mjitie katika kuwahudumia watu kama hawa na kila mmoja aingiaye kwenye kazi na kuifanya kwa bidii. \v 17 Nilifurahi Stefana, Fortunato na Akaiko walipofika, kwa sababu wamenipatia yale niliyopungukiwa kutoka kwenu. \v 18 Kwa kuwa waliiburudisha roho yangu na zenu pia. Watu kama hawa wanastahili kutambuliwa. \b \s1 Salamu za mwisho \p \v 19 Makundi ya waumini wa jimbo la Asia wanawasalimu. \p Akila na Prisila\f + \fr 16:19 \fr*\ft kwa Kiyunani ni \ft*\fqa Priska\fqa*\f* pamoja na kundi la waumini walioko nyumbani mwao wanawasalimu sana katika Bwana Isa. \p \v 20 Ndugu wote walio hapa wanawasalimu. Salimianeni kwa busu takatifu. \b \p \v 21 Mimi, Paulo, naandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe. \b \p \v 22 Kama mtu yeyote hampendi Bwana Isa Al-Masihi, na alaaniwe. Bwana wetu Isa, njoo\f + \fr 16:22 \fr*\ft kwa Kiaramu ni \+tl Marana tha\+tl*\ft*\f*. \b \p \v 23 Neema ya Bwana Isa iwe nanyi. \b \p \v 24 Upendo wangu uwe nanyi nyote katika Al-Masihi Isa. Amen.